SONYA_FLAWLESS_IMG
WE CREATE GREATNESS. | Professional Networker | Global Business Builder | Health And Wellness Coach | YOUR DREAM OUR PLAN.

Thursday, January 2, 2014

Rais Jakaya Kikwete:“Tunakamilisha matayarisho ya kuanza awamu ya pili ya Operesheni Tokomeza. Ni muhimu kuendelea nayo kwani tusipofanya hivyo majangili wataendelea na vitendo vyao viovu.

Rais Jakaya Kikwete
----
Rais Jakaya Kikwete amesema Operesheni Tokomeza Ujangili iliyositishwa kwa muda kutokana na utekelezaji wake kukumbwa na kasoro na kusababisha mawaziri wake wanne kuwajibika kisiasa, itaendelea baada ya kukamilika kwa matayarisho ya awamu yake ya pili.

Akizungumza katika salamu zake za Mwaka Mpya jana, Rais Kikwete alisema:  “Tunakamilisha matayarisho ya kuanza awamu ya pili ya Operesheni Tokomeza. Ni muhimu kuendelea nayo kwani tusipofanya hivyo majangili wataendelea na vitendo vyao viovu.

“Wakati nikilihutubia Bunge Novemba 7, mwaka jana niliagiza ifanyike sensa katika Pori la Hifadhi la Selous. Hali ni mbaya, sensa imekamilika lakini taarifa yake inatisha. Kuna tembo 13,084 tu wakati mwaka 1976 walikuwa na tembo 109,419.”

Rais Kikwete ametoa kauli hiyo ikiwa zimepita siku 12 tangu Kamati ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Mazingira ilipotoa ripoti yake iliyoeleza athari mbalimbali za operesheni hiyo, ikiwa ni pamoja na unyanyasaji, uharibifu wa mali na mauaji ya binadamu na mifugo.

Ripoti hiyo ilisababisha, Rais kutengua uwaziri wa Dk Emmanuel Nchimbi (Mambo ya Ndani), Shamsi Vuai Nahodha (Ulinzi), Dk David Mathayo (Mifugo na Uvuvi) na Balozi Khamis Kagasheki (Maliasili na Utalii), baada ya wizara zao kutajwa kushindwa kusimamia utekelezaji wa operesheni hiyo.

Hata hivyo, Rais alisema mtindo wa mzigo wa makosa ya watumishi wa umma kubebwa na viongozi wa kisiasa pekee, tena wasiokuwa na hatia ya moja kwa moja, siyo sahihi. “Lazima kila mtu abebe mzigo wake inavyostahili. Ni matumaini yangu pia kwamba katika siku za usoni kunapotokea matatizo ya namna hii uchunguzi uwe wa kina ili wale hasa waliohusika na kutenda makosa wawajibishwe.
Kwa Habari zaidi Bofya na Endelea......

0 comments:

Post a Comment