SONYA_FLAWLESS_IMG
WE CREATE GREATNESS. | Professional Networker | Global Business Builder | Health And Wellness Coach | YOUR DREAM OUR PLAN.

Wednesday, January 8, 2014

Mkurugenzi wa Mkurugenzi wa Mamlaka ya Usafiri wa Barani Zanzibar(ZMA)Abdi Omar Alipozungumza na Waandishi na kutoa Majina ya Watu waliopetea na Waliookolewa kwenye ajali ya Boti ya kilimanjaro iliyonusurika kuzama

 Mkurugenzi wa Mamlaka ya Usafiri wa Barani Zanzibar Bwa.Abdi Omar akizungumza na Waandishi wa habari wa Vyombo mbalimbali kuhusiana na zoezi la uokoaji lililoendelea leo asubuhi katika eneo la tukio katika mkondo wa bahari wa Nungwi.
Sehemu ya Waandishi wa habari wa Vyombo mbalimbali wakimsikiliza Mkurugenzi wa Mamlaka ya Usafiri wa Barani Zanzibar Bwa.Abdi Omar(hayupo pichani)kuhusiana na zoezi la uokoaji lililoendelea leo asubuhi katika eneo la tukio katika mkondo wa bahari wa Nungwi.
---
Na Mwaandishi Wetu.
Mkurugenzi wa Mamlaka ya Usafiri wa Barani Zanzibar Bwa.Abdi Omar akizungumza na Waandishi wa habari wa Vyombo mbalimbali kuhusiana na zoezi la uokoaji lililoendelea jana asubuhi katika eneo la tukio katika mkondo wa bahari wa Nungwi.

Amesema katika Na kusema katika zoezi la jana  hakuna mtu yoyote aliyepatikana wati wa zoezi hilo na zoezi hiloliloaza asubuhi ya leo hakuna mafanikio ya kupata miili iliopata ajali hiyo, hadi mchana wa leo hali imekuwa hivyo na bado zeizi linaendele ili kupata miili ambayo mpaka sasa jamaa zao wamejitokeza kutokana na jamaa zao kupotea katika maafa hayo.

 Zoezi hilo linaendelea chini ya Vikosi vya Serekali na Wananchi wa Nungwi  ili kupata  Wananchi waliopotea katika ajali hiyo.

Amewataja  Abiria waliookolewa katika ajali hiyo jana mchana ambao wamepatikana Watu watatu ambao ni Nahir Ali Issa  Mwamme mkaazi wa Mtoni Jeshini Unguja, Ali Maulid Haji mkaazi wa mtoni jeshini Unguja na Ali Salim Ali mkaazi wa Vitongoji kisiwani Pemba .

Pia amatowa majina ya Jamaa zaowamefika katika Idara yake kutoa taarifa ya mpaka sasa jamaa zao hawajawaona kutoka na ajali hiyo walikuwa katika boti hiyo ya Kilimanjaro wakitokea Pemba kwani Mohammed Khamis Said, (13) mkaazi wa Kibweni Unguja, Najma Salum, (13) Nahid Khamis Issa, (5) Adam Nassor Mohammed (13) Suleiman Mbarouk Salum, Mohammed Said Ali, Sumaiya Said Ali, na Sama Ali  Juma.

Mpaka sasa  Wananchi wa jamaa hawa wamefika katika Ofisi za ZMA kujitambulisha kukosa jamaa zao walikuwa katika Boti hiyo wakati ikitokea kisiwani Pemba ikiwa katika safari zake za kawaida na kupata mkasa wa dharuba ya upepo katika mkondo wa Nungwi na baadhi ya abiria waliokuwa wamekaa katika sehemu ya mbele ya boti hiyo kuchukuliwa na wimbi na kutoswa baharini.

Amesema zoezi hilolinaendelea katika jitihada za kutafuta Wananchi waliokuwa taika Boti hiyo katika sehemu ya bahari ya Zanzibar na sehemu nyegini ili kuhakikisha wanafanikiwa kupata Wananchi waliohusika na ajali hiyo kukasbidhi kwa jamaa zao

0 comments:

Post a Comment