SONYA_FLAWLESS_IMG
WE CREATE GREATNESS. | Professional Networker | Global Business Builder | Health And Wellness Coach | YOUR DREAM OUR PLAN.

Friday, January 3, 2014

GEBI PRESHA YAIFUNGA CLOUDS MEDIA 2-1

 Winga Machachali wa Timu ya Clouds Media,Said Tully akituliza mpira kwa umaridadi kabisa mbele ya Beki wa Timu ya Gebi Presha ya Magomeni wakati wa Mtanange wao wa kufunga mwaka,uliofanyika kwenye Uwanja wa Tanganyika Packers,Kawe jijini Dar.Clouds Media walilala kwa mabao 2-1
Mshambuliaji wa Timu ya Gebi Presha ya Magomeni,akiondoka na mpira.
Ilikuwa ni patashika la nguvu uwanjani hapo.
Dukiiiiiiiiii........
Hatariii langoni mwa timu ya Clouds Media.
Kiungo mshambuliaji wa timu ya Clouds Media, Shaffih Dauda akiipangua ngome ya Gebi Presha.
haya twendeeeee......
Kocha wa timu ya Clouds Media, Alex Lwambano akiwa ameshika kiuno baada ya timu yake kupigwa bao 2,huku akiwa na mashaka tele juu ya kibarua chake katika timu yake hiyo.maana hii ilikuwa ni mechi ya pili kupigwa,tena nyumbani.
Kocha Lwambano akiongea kwa unyonge na wachezaji wake ili wajitahidi kukaza.
Kocha Lwambano akitoa maelekezo kwa wachezaji wa timu yake wakati wa mchezo huo.
Kwa Upande wa Gebi Presha kulikuwa na makocha wa kutosha tu,kwani kila mmoja alitoa mawaidha kwa mchezaji wake.labda ndio maana wakaibuka kidedea.
Makocha wakimwaga cheche kwa wachezaji wao.
Umesikia wewe........
Straika Antonio Nugaz akiondoka na kijiji.
Mashabiki lukuki.

0 comments:

Post a Comment