SONYA_FLAWLESS_IMG
WE CREATE GREATNESS. | Professional Networker | Global Business Builder | Health And Wellness Coach | YOUR DREAM OUR PLAN.

Friday, October 11, 2013

Rais Banda Amewafuta Kazi Mawaziri Wake Wote Kutokana Na Ufisadi

Rais wa Malawi, Joyce Banda.
Rais wa Malawi, Joyce Banda amelifuta kazi baraza lake la mawaziri kutokana na kuongezeka kwa visa vya ufisadi serikalini.

Maafisa wa serikali wamekuwa wakipatikana na pesa zikiwa zimefichwa chini ya vitanda vyao na kwenye magari yao, kwa mujibu wa mwandishi wa BBC Raphael Tenthani.
Mwezi jana afisaa mmoja mkuu katika wizara ya fedha Paul Mphwiyo, aliyeonekana kuwa afisaa mmoja mkuu serikali ambaye anaonekana kupinga sana ufisadi, alipigwa risasi na kujeruhiwa.
Wahisani wa kimataifa wamekuwa wakimtaka rais Banda kuchukua hatua kukabiliana na ufisadi.
Malawi ni taifa masikini na hutegemea sana msaada kutoka kwa Muungano wa Ulaya na nchi zengine za kimagharibi.
Bi banda amesema kuwa mawaziri wapya watateuliwa hivi karibuni bila ya kutoa maelezo zaidi.
Aliitisha mkutano wa dharura wa baraza la mawaziri kabla kutangaza kulivunja.
Kwenye mkutano na waandishi wa habari Banda alisema kuwa ameunda jopo maalum likijumuisha polisi na maafisa wa serikali kufanya ukaguzi wa matumizi ya pesa za serikali katika idara zote za serikali.
Mwandishi wa BBC nchini humo anasema kupigwa risasi kwa bwana Mphwiyo ndio ilikuwa mwanzo wa taarfa kuwa baadhi ya maafisa wa serikali wanashirikiana na wafanyabisahara kuifilisi serikali katika utoaji wa kandarasi na mikataba bandia.
Washukiwa wanne walikamatwa kuhusiana na kupigwa risasi kwa afisa huyo.
Takriban maafisa kumi wa serikali wama
ekamatwa wakisubiri kusikilizwa kwa kesi zao kuhusiana na ufisadi.
CHANZO: BBC SWAHILI

0 comments:

Post a Comment