Agnes Gerald (Masogange)
---
Mtanzania Agnes Gerald, maarufu Masogange, ameachiwa huru na
Mahakama ya Kempton ya jijini Johannesburg, baada ya kulipa faini ya
R30,000 (Sh4.8 milioni) kwa kosa la kubeba kemikali zinazotumika
kutengeneza dawa za kulevya.
Wakati Masogange akitozwa faini hiyo mwenzake,
Melissa Edward ameachiwa huru na mahakama hiyo, baada ya kukosekana
ushahidi wa kumtia hatiani.
Msemaji wa Kitengo cha Uchunguzi wa Makosa ya
Jinai cha Afrika Kusini(Hawk), Kapteni Paul Ramaloko alisema Watanzania
hao wameachiwa huru baada ya kuonekana kuwa hawakubeba dawa za kulevya,
bali kemikali aina ya ephedrine.
Hata hivyo, Mahakama ilibaini kuwa, Melissa hana
hatia kwa kuwa ilionekana kuwa amemsindikiza Masogange, ambaye alimwomba
amsaidie kubeba mzigo huo.
“Mahakama iliona kuwa Melissa aliombwa tu
kumsaidia kubeba baadhi ya mabegi, lakini hayakuwa yake. Mizigo yote
iliandikwa jina la Agness Gerald na si Melissa,” alisema Kapteni
Ramaloko.
Kwa Habar iZaidi




0 comments:
Post a Comment