SONYA_FLAWLESS_IMG
WE CREATE GREATNESS. | Professional Networker | Global Business Builder | Health And Wellness Coach | YOUR DREAM OUR PLAN.

Monday, April 29, 2013

EXTRA BONGO YAZIDI KUWABAMBA MASHABIKI NDANI YA MEEDA SINZA

Mkurugenzi wa Extra bongo Ally Choki akiimba mbele ya mashabiki wake (Hawapo Pichani) ndani ya Ukumbi wa Meeda sinza juzi Usiku wakati bendi yake ilipokuwa ikiburudisha pande pande hizo
Kushoto ni mwimbaji mahiri wa bendi ya Extra Bongo Athanas akiwa na Mwimbaji pekee wa kike wa bendi hiyo Khadija Mnoga a.k.a "Kimobitel" ambaye anatamba kwa sasa na wimbo wake wa "Mgeni" wakishoo luv mbele ya kamera yetu ndani ya ukumbi wa Meeda Sinza juzi usiku wakati Bendi yao ilipokuwa ikitumbuiza pande hizo.
Kushoto ni mmoja wa marapa bora wa muziki wa dansi Totoo Ze Bingwa akirap ndani ya Meeda sinza wakati Bendi anayopigia mzigo Extra Bongo ilipokuwa ikitumbuiza pande hizo na kulia ni Banza Stone a.k.a Generale akimpa big up.
Maua ya Extra Bongo mzigoni
Wakata nyonga maarufu kwa sasa wa Extra bongo wakiongozwa na nyamwela wakiwapagawisha mashabiki waliohudhuria shoo hiyo ndani ya Meeda Sinza juzi usiku
Waimbji bora wa Extra bongo kulia ni Rogert Hega a.k.a Katapila wakiimba ndani ya Meeda Sinza juzi usiku
Rapa bora wa Extra bongo Kabatano (Kulia) akigani moja ya jimbo zao bora huku akipewa sapoti na nguli wa muziki wa dansi Banza Stone mwana masanja wakati bendi hiyo ilipokuwa ikitumbuiza maeneo ya Sinza katika ukumbi wa Meeda juzi usiku.

0 comments:

Post a Comment