SONYA_FLAWLESS_IMG
WE CREATE GREATNESS. | Professional Networker | Global Business Builder | Health And Wellness Coach | YOUR DREAM OUR PLAN.

Tuesday, November 29, 2011

ULE WARAKA WA CHADEMA KWA RAIS JAKAYA KIKWETE JUU YA SHERIA YA MABADILIKO YA KATIBA, 2011

Rais Jakaya Mrisho Kikwete akisikiliza maelezo toka kwa Mwenyekiti wa CHADEMA Mh. Freeman Mbowe baada ya kupokea  mapendekezo ya chama hicho juu ya kuundwa katiba mpya yatayozungumzwa kwenye mkutano huo wa kihistoria uliofanyika juzi Ikulu jijini Dar es salaam
--
Mheshimiwa Rais,
 
Sisi ambao majina yetu yameambatanishwa chini ya Waraka huu tunakuandikia, kwa niaba ya Kamati Kuu ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), kukushauri kutumia mamlaka yako chini ya ibara ya 97(2) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano kukataa kuukubali Muswada waSheria  ya  Mabadiliko  ya  Katiba  ya  mwaka  2011  uliopitishwa  na  Bunge  la
 
Jamhuri ya Muungano tarehe 18 Novemba, 2011. Sheria hiyo sasa inasubiri ridhaa yako Mheshimiwa Rais kabla ya kuanza kutumika.Ushauri wetuunatokana na imani yetu endapo Muswada huu utapata ridhaa yako na kuanza kutumika kama Sheria utakuwa na madhara makubwa kwa mchakato mzima wa utungaji wa Katiba Mpya na amani na utulivu wa nchi yetu kwa sababu zifuatazo zitokanazo na Muswada wenyewe.
 
USHIRIKISHWAJI HAFIFU WA WABUNGE NA  WANANCHI 
           
Mheshimiwa Rais, .  
Muswada wa  Sheria ya Mabadiliko ya Katiba ulichapishwa kwa mara ya kwanza kwenye Gazeti la Serikali la tarehe 11 Machi 2011.Muswada huo ulipelekwa katika Mkutano wa Tatu wa Bunge la Jamhuri ya Muungano kwa Hati ya Dharura tarehe 9 Aprili 2011. Hata hivyo, baada ya upinzani mkubwa dhidi ya Muswada huo kujitokeza karibu nchi nzima, Bunge lililazimika kuondoa Hati ya Dharura na hivyo kufanya Muswada kushughulikiwa kwa mujibu wa utaratibu wa kawaida wa kutunga sheria uliowekwa na Kanuni za Kudumu za Bunge.

Katika kufanya hivyo, Bunge liliiagiza Serikali kufanya mambo yafuatayo kwa mujibu wa Taarifa Rasmi ya Majadiliano Katika Bunge ya tarehe 15 Aprili 2011:Kusoma Zaidi Waraka Huu Bofya na Endelea.........>>>>>>>

0 comments:

Post a Comment