Rais Jacob
Zuma wa Afrika Kusini amesema kuwa, maandalizi na uendeshwaji muruwa wa
mashindano ya kombe la dunia umeliamsha bara la Afrika na kuudhihirishia
ulimwengu kuwa hata nchi zinazoendelea zinaweza kuandaa matukio muhimu
ya dunia. Akizungumza kwenye mahojiano na kitengo cha habari cha FIFA
Zuma amesema kuwa kutokana na tadbiri ya nchi yake kwenye mashindano ya
kombe la dunia, sasa pana haja ya bara hili kupewa fursa nyingine ya
kuandaa mashindano ya Olimpiki. Amesema kuwa ana matumaini makubwa kuwa
bara hili litatunukiwa heshima ya kundaa Olimpiki siku za usoni.




0 comments:
Post a Comment