
Mkurugenzi wa Uchumi Mdhibiti wa Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (Ewura), Felix Ngamlagosi akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam jana, alipokuwa akitangaza viwango vipya vya bei ya umeme. Kulia ni Mkurugenzi wa Umeme wa mamlaka hiyo, Anastas Mbawala. Picha na Silvan Kiwale
Tarehe 11 Oktoba 2013, Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) liliwasilisha maombi ya kurekebisha bei ya umeme kwa Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA). TANESCO ilipendekeza kuongeza bei kwa asilimia 67.87 kuanzia tarehe 1 Oktoba 2013, asilimia 12.74 kuanzia tarehe 1 Januari 2014 na asilimia 9.17 kuanzia tarehe 1 Januari 2015.



