JEURI ya pesa. Ndicho unachoweza
kusema baada ya klabu tajiri Ulaya, Paris Saint-Germain na Manchester
City kudaiwa kuwa zipo tayari kumng'oa, Lionel Messi, kutoka Barcelona
kwa gharama yoyote ile. Wakati ikiwekwa wazi kwamba thamani ya
supastaa huyo wa Kiargentina ni Euro 400 milioni, klabu hizo
zinazomilikiwa na matajiri wenye pesa ndefu, zimesema zipo tayari.