SONYA_FLAWLESS_IMG
WE CREATE GREATNESS. | Professional Networker | Global Business Builder | Health And Wellness Coach | YOUR DREAM OUR PLAN.

Wednesday, July 16, 2014

Neno Fupi La Leo: Uafrika Ni Imani

Ndugu zangu,

Uafrika ni imani. Uafrika umejijenga katika upendo na ujamaa. Ndio maana Mwalimu aliijenga TANU na nchi yetu katika misingi ya Ujamaa wa Kiafrika, hivyo basi itikadi. Ni tofauti kabisa na Ukomunisti.

Mathalan, Afrika unapokuwa safarini na jua likazama, basi, Mwafrika hutafuta yalipo makazi ya watu. Afrika safari zetu nyingi ni za miguu, na kwa kawaida hatutembei usiku.

Na jua likizama na ukakutana na Mwafrika mwenzako kwenye mji wake, husemi kuwa unataka kusaidiwa pa kulala na mengineyo. Kwa mila zetu, utasema; " Mwenzenu niko safarini na jua limezama nikiwa hapa". 

Kwa Mwafrika, hapo umehitaji msaada. Mwenyeji ataandaa pa wewe kulala. Utaandaliwa chakula na hata maji ya moto ya kuoga. Atakayefanya ukarimu huo hatajali kama wewe ni Mkristo, Muislamu, au wa kabila tofauti na yeye.
 
Na asubuhi kukipambazuka, utapewa kijana wa kukusindikiza kilomita zipatazo mbili. Uendelee na safari yako.

Ndio, Uafrika ni imani iliyojengeka katika misingi ya upendo, umoja na kusaidiana bila kubaguana.
 
Ni Neno Fupi La Leo
Maggid Mjengwa,
Iringa.

0 comments:

Post a Comment