SONYA_FLAWLESS_IMG
WE CREATE GREATNESS. | Professional Networker | Global Business Builder | Health And Wellness Coach | YOUR DREAM OUR PLAN.

Tuesday, July 6, 2010

WATANZANIA WACHUKUA NONDOZ ZAO HYDERABAD(INDIA)!!!
NI siku ya furaha katika maisha ya wanafunzi waliohitimu shahada zao za kwanza elimu ya juu hapa Hyderabad-India.Wakirusha kofia zao juu kuashiria kuhitimu kwao
Wahitimu wakipata picha ya pamoja na Mgeni Rasmi Pr.V.RAMA RAO mkuu wa chuo cha Aptech India pamoja na Mwenyekiti wa Jumuiya ya Watanzania wote waishio Hyderabad Bw.ABDILLAH D. NKYA.
Picha za pamoja ulikuwa ni mtindo wa kubadilishana nafasi kama unavyoonekana hili wote wapate nafasi ya kupata kumbukumbu
Wa kwanza kutoka kushoto ni Bw.MUSTAFA SAID(a.k.a MATATA ) akiwa na Bw.NASSIB pamoja na Bw.SADDALLAH R. MBEYU wakipata kumbukumbu ya pamoja katika mahafali hayo.
Bw. MOHAMED KHAMIS akiwa na Bw.Matata akipata picha ya kumbukumbu.
Bw.MATATA akipokea cheti chake akiashiria amani na upendo.

Bw.NASSIB nae akipokea chati chake kwa kuwa mwanafunzi wa kwanza kwa kuandaa jarida kwa wahitimu kitu ambacho hakijawahi kutokea katika historia ya wanafunzi wasomao hapa Hyderabad,kazi nzuri sana
Bw.KHALID SAID BAHASAN ni mmoja ya wahitimu kwa mwaka huu akipokea cheti chake toka kwa mgeni rasmi.
Bw.SADALLAH MBEYU akionesha cheti chake juu akiasiria hiki hapa cheti jamani mmekiona.
Bw.SADALLAH MBEYU akiwa na Bw.MATATA katika picha ya pamoja wakiwa ndani ya ukumbi wa mahafali huku wakisikiliza nini kinaendeleaa toka kwa mshereheshaji.
Mwenyekiti wa Jumuiya ya wanafunzi wanaoishi hapa Hyderabad Bw.ABDILLAH D. NKYA akiwa na Mgeni Rasmi katika maafali Pr.V RAMA RAO
Baadhi ya sehemu ya wageni waalikwa waliofika katika mahafali hayo pia wakiwa ni wanafunzi waliohudhuria kwa kuwasindikiza wahitimu kwa kumaliza mda wao wa masomo hapa Hyderabad-India.
Ulikuwa ni muda wa kuimba wimbo wa Taifa wa Tanzania kama ilivyokawaida katika kila shughuli zetu tulisimama na kuimba kwa pamoja

Baadhi ya sehemu ya wageni waalikwa wakiimba wimbo wa Taifa wa Tanzania

Wahitimu nao wakiimba wimbo wa Taifa kwa pamoja
Wahitimu wakiwa katika nyuso za tabashashi kabisaa katika kuimba wimbo wa Taifa

Baadhi ya wahitimu wakiimba wimbo wa Taifa kwa heshima zote
Mwenyekiti wa Jumuiya wa Watanzania akiwa na Mgeni Rasmi mbele kabisa wakiwa katika heshima zote kwa kuimba wiimbo wa Taifa
Bw.SADALLAH MBEYU

Wahitimu wakiwa kimya nia baada ya kumaliza kuimba wimbo wa Taifa
Mbele kabisa Bi.FATMA SALUM akifuatiwa na Bi.KHADIJA NASSOR wakiwa katika nyuso za furaha kabisa katika kuwasindikiza wenzao.
Bw.Nass akitafakari jambo na Bw.Deuce Majige katika mahafali hayo
Bw.SHAKIR wa kwanza toka kushoto akiwa na Bw.IBRAHIM wakipata kumbukumbu ya pamoja katika mahafali hayo hapa ni nje ya ukumbi
Hawa ni baadhi ya wahitimu mbele kabisa ni Bw.Walid akifuatiwa na Bw.Anwar mwisho wao ni Bw.Daniel Masimbusi
Hapa ni Bw. ABDULAZIZ akiashiria jambo fulani.

MOHAMED KHAMIS akipata picha ya pamoja na mmoja wa wahitimu Bw.ANWAR na mwisho kabisa ni Bw.NASSIB.
Mbele kabisa ni Bw.Abdulaziz akifuatiwa na Bw.Walid na mwisho kwa mbali ni Bw.Noor wakipata chai ndani ya ukumbi
Hapa ni kabla ya tukio maeneo ya SAINKPUR
Bw. SAID MIHALA mwenye kofia akibadilishana mawili matatu na Bw. ALLY.

Bw.SUNDAY wa kwanza toka kulia(mwenye tai) akiwa na Bw.SAID MIHALA na Bw. ALLY hapa ni ndani ya ukumbi
Mwenye T-Shirt nyekundu ni mhitimu Bw. ANWAR akiwa na Mwanaharakati wa blog hii
mwenye miwani kifuani Bw. ALLY. 
Mwisho nawatakieni kila la kheri wahitimu wote kwa kumaliza salama muda wenu wote wa masomo yenu na kufanikiwa kuhitimu, nawatakieni maisha mema yenye mafaniko tele huko muendako mkayafanyie kazi yale yote ambayo mmejifunza kivitendo ili tuweze kulisukuma gurudumu la Taifa letu mbele,
MWENYEZI MUNGU AWABARIKI!!!!
Imeandikwa na ALLY S. MGIDO'S

0 comments:

Post a Comment