SONYA_FLAWLESS_IMG
WE CREATE GREATNESS. | Professional Networker | Global Business Builder | Health And Wellness Coach | YOUR DREAM OUR PLAN.

Thursday, December 1, 2011

KITUO CHA TIMES RADIO FM YAZALIWA UPYA

Mmoja wa watangazaji wa Times Radio FM, Ali Masoud 'Kipanya'  akiongoza hafla hiyo.
Mtangazaji wa TIME FM, Scolastica Mazula (kulia) akiwa na baadhi ya wageni waalikwa.
Mkurugenzi Mtendaji wa Kituo cha Times Radio FM, Rehule Nyaulawa akielezea historia na mafanikio ya kituo hicho, wakati wa hafla ya kukitambulisha upya kituo hicho, Dar es Salaam jana.Kituo hicho kilichoanzishwa mwaka 2000, hivi sasa kinaongoza kusikilizwa na watu wengi katika mikoa ya Dar es Salaam, Pwani na Morogoro.
Baadhi ya wageni waalikwa wakiwa katika hafla hiy, iliyofanyika kwenye Hoteli ya Kilimanjaro, Dar es Salaam.
Mkurugenzi Mtendaji wa Kituo cha Times Radio FM, Rehule Nyaulawa (katikati), akiwa na aliyemwakilisha mgeni rasmi, Sihaba Nkinga (wa pili kulia) pamoja na baadhi ya wageni waalikwa.
Mkurugenzi Mtendaji wa Kituo cha Times Radio FM, Rehule Nyaulawa  (kulia) akigana na Naibu Katibu Mkuu wa wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Sihaba Nkinga baada ya hafla hiyo kumalizika.
Na H@ki Ngowi

0 comments:

Post a Comment