Msanii
wa kizazi kipya anaekuja juu kwa sasa aitwaye Ben Paul akiimba kwa
hisia jukwaani mbele ya mashabiki wa tamasha la msimu wa dhahabu
unaoendelea na serengeti fiesta 2011 jioni ya Jana kwenye uwanja wa
Kambarage,ambapo wakazi wa Shinyanga walijitokeza kwa wingi.
Kicha
mahiri katika miondoko ya Hip hop Bongo,Farid Kubanda a.k.a Fid Q
akikamua jukwaani jioni ya jana kwenye tamasha la Serengeti fiesta
2011.Tamasha la Serengeti Fiesta linaandaliwa na kampuni bingwa ya
Burudani hapa nchini ya Prime Time Promotions Ltd ikishirikiana na
Clouds Media Group,wakati huo huo mdhamini mkubwa wa tamasha hilo ni
kampuni ya bia ya Serengeti Breweries Ltd kupitia kinywaji chake
maridhawa kabisa,Serengeti Primeum Lager.
Mkali mwingine wa hip hop Bongo akitokea jijini Arusha,JCB akiwaangushia madini wakazi wa shinyanga jioni ya jana
Baba Jonii Adam Mchomvu nae alikuwepo kuwiambisha wakazi wa Shinyanga
Mzee
wa Robo saa a.k.a Amin kutoka THT akitumbuiza jukwaani na baadhi ya
nyimbo zake ikiwemo ya robo saa,bora nikimbie pamoja singo yake mpya
iitwayo Mapenzi yameteka Dunia.
Msanii
mahiri wa kizazi kizazi kipya,Mwasiti akiimba pamoja na shabiki wake
jukwaani jioni ya jana ndani ya uwanja wa kambarage wakati wa tamasha la
Serengeti Fiesta 2011 likiendelea.
Mheshimiwa Themba akicheza na shabiki ambaye aliomba apande jukwaani nae ajiachie pamoja na ulemavu wake.
Baadhi
ya wasanii wa mkoani Shinyanga wakiwa jukwaani mchana huu tayari kwa
amsha amsha kwa tamasha la Serengeti Fiesta 2011 ndani ya uwanja wa
Kambarage,
Kutoka
Kiumeni,Wasanii mahiri wa bongofleva Chege na Themba pichani juu na
chini wakiwaimbisha wakazi wa Shinyanga kwa namna ya kipekee kabisa
jioni ya jana kwenye tamasha la Serengeti fiesta ndani ya uwanja wa
Kambarage,ilikuwa ni full kushangweka bila Majotro kabisa.
Aahhhhhh mbona kwa sana tuu....kitu cha Golden moment kipo hapa.
Shinyanga nayo aaaahhhh....!haina majotro kabisaa.
Mmoja
wa watangazaji mahiri wa Clouds FM/TV pichani kulia Wasi Wasi
Mwambulambo akiwa na fundi mitambo, Dj Haroun wa Prime Time Promotions
Ltd mchana huu ndani ya Uwanja wa Kambarage tayari kwa kulianzisha
tamasha la Serengeti Fiesta 2011.
Ni Full kushangweka kama kawa wala haina majotro kwa wakazi wa Shinyanga.
Baadhi
ya Wafanyakazi wa Kampuni ya SBL mkoani Shinyanga wakijipanga vyema
mikakati ya mauzo ya vinywaji vya kampuni hiyo kwa wateja wao.
0 comments:
Post a Comment