Makamu
wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal,
akikata utepe kuzindua rasmi huduma mpya ya Mfumo wa Utambuzi wa Bidhaa
Tanzania, (Global Standard 1 ), wakati wa uzinduzi huo uliofanyika
kwenye Viwanja vya Mwalimu Julius Nyerere leo Julai 04, 2011.
Makamu
wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal,
akisoma hotuba yake wakati wa uzinduzi wa Huduma Global Standard GS1
nchini Tanzania, ‘Mfumo wa utambuzi wa Bidhaa’Uliozinduliwa leo Julai
04, 2011 kwenye Viwanja vya Julius Nyerere Dar es Salaa.
Makamu
wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal,
akisalimiana na Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar, Maalim Seif
Sharif Hamad, wakati walipokutana kwenye viwanja vya Mwalimu Julius
Nyerere katika Maonyesho ya 35 ya Biashara ya Kimataifa leo Julai 04,
2011.
Makamu
wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, DKt. Mohammed Gharib Biala,
akisikiliza maelezo ya mjasiliamali, Angela John, kuhusu mashine ya
Kusokota, wakati alipotembelea katika Banda la Sido kwenye Maonyesho ya
35 ya Biashara ya Kimataifa yanayoendelea katika Viwanja vya Mwalimu
Julius Nyerere
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib
Bilal, akisikiliza maelezo kutoka kwa Mkurugenzi mtendaji wa Kampuni ya
Power Electronics & Controls Ltd, Kayungi Kayungi, kuhusu Mashine
ndogo inayozalisha Umeme kwa kutumia maji, wakati alipotembelea Banda la
Sido kwenye Maonyesho ya 35 ya Biashara ya Kimataifa yanayoendelea
katika Viwanja vya Mwalimu Julius Nyerere Dar es Salaam.
Picha na
Muhidin Sufiani-Ofisi Ya Makamu wa Rais
0 comments:
Post a Comment