SONYA_FLAWLESS_IMG
WE CREATE GREATNESS. | Professional Networker | Global Business Builder | Health And Wellness Coach | YOUR DREAM OUR PLAN.

Wednesday, July 6, 2011

Ombi La Liverpool Lakataliwa Na Villa

Stewart Downing mchezaji wa kiungo cha kati wa Aston Villa
Klabu ya Aston Villa, imekataa ombi la Liverpool la kuitaka kumsajili mchezaji wake Stewart Downing kwa kitita cha £15m.
BBC imegundua kuwa klabu ya Aston Villa, inataka kulipwa kitita cha £20m ili kukubali uuzaji wa mchezaji huyo wa timu ya taifa ya Uingereza mwenye umri wa miaka 26.
Stewart ambaye alijiunga na Villa kutoka kwa klabu ya Middlesbrough kwa kitita cha £12m mwaka wa 2009, hajaafikiana na kocha wake Alex McLeish kuhusu kandarasi mpya na duru zinasema kuwa kocha huyo yuko tayari kumuuza stewart.
Mchezaji huyo wa kiungo cha kati pia amehusishwa na klabu ya Arsenal, lakini Liverpool ina nafasi nzuri ya Kumsajili.
Habari zaidi zinaendelea kujitokeza.

0 comments:

Post a Comment