Mkuu
wa mauzo wa kitengo cha Vodacom m-pesa Franklin Bagalla kushoto
akitoa maelezo kwa waandishi wa habari njia zinazotumika kulipia kodi
kupitia huduma ya m-pesa ,katikati ni Naibu Kamishina Mkuu wa Mamlaka
ya Mapato Tanzania (TRA) Placidus Luoga,na Mkurugenzi wa Fedha TRA
Saleh Mshoro ,Kampuni ya Vodacom kushirikiana na Mamlaka ya mapato
Tanzania(TRA) jana imetanagza rasmi kuanza kutumika kwa njia hiyo ya
m-pesa kulipia kodi.
Naibu
Kamishina Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Placidus Luoga
akisisitiza jambo kwa waandishi wa habari wakati wa utambulisho rasmi
wa huduma ya malipo ya kodi kupitia Vodacom m-pesa inayotolewa na
kampuni ya Vodacom Tanzania, kulia ni Mkurugenzi wa Fedha wa Mamlaka
ya mapato Tanzania Saleh Mshoro na kushoto ni Mkuu wa Mauzo wa Vodacom
m-pesa Franklin Bagalla.
Mkuu
wa kitengo cha Mahusiano wa kampuni ya Vodacom Tanzania Nector Foya
katikati akiwaonyesha Naibu Kamishina Mkuu wa Mamlaka ya Mapato
Tanzania (TRA) Placidus Luoga,na Mkuu wa kitengo cha Mauzo Vodacom
m-pesa FranklinBagalla bango litakalotumika kuelimisha umma njia za
ulipaji kodi kupitia huduma ya Vodacom m-pesa wakati wa utambulisho
rasmi wa huduma hiyo kwa waandishi wa habari jana jijini dare s salaam.
TRA kukusanya kodi kwa Vodacom m-pesa
Dar es Salaam June 13, 2011
Kampuni ya simu za mkoni ya Vodacom Tanzania kwa kushirikiana na TRA
zimetangaza huduma mpya ya ukusanyaji kodi huduma hiyo ni ya njia ya m-pesa
inayotolewa na Vodacom Tanzania ambapo walipiaji wa kodi nchini
wanaweza kulipia kodi na ada mbalimbali za leseni za udereva kupitia
simu zao za mkononi.
Kuanzishwa
kwa huduma hiyo ni mwendelezo wa azma na dhamira ya kampuni ya kamuni
hiyo katika kubuni huduma bora zenye kuongeza thamani ya simu za mkononi
kwa lengo la kuleta mapinduzi katika sekta ya mawasiliano ya simu za
mkononi nchini.
Huduma hiyo mpya ya kulipia kodi kwa m-pesa
inahusisha malipo ya kodi ya majengo, kodi ya mapato na malipo ya ada
mbalimbali za leseni za udereva ambayo ni matokeo ya ushirikiano wa
kampuni ya Vodacom na Mamlaka ya Mapato Tanzania – TRA.
“Tunapenda
kuwatangazia umma mapinduzi mengine ya aina yake katika huduma ya
m-pesa ambapo kuanzia sasa walipaji wa kodi hawatakuwa na sababu ya
kuhofia njia rahisi ya kutimiza wajibu wao wa kulipa kodi kwani kupitia m-pesa wanaweza kufanya hivyo kwa urahisi, usalama na uhakika zaidi”Alisema Mkuu wa Mauzo wa m-pesa Bw Franklin Bagalla.
Ili mlipa kodi aweze kutumia huduma hiyo atapaswa kuwa mteja wa Vodacom aliyejisajili na huduma ya m-pesa na kisha kuzingatia taratibu za kawaida za kuingia na kutumia mfumo wa m-pesa kwenye simu yake ya mkononi na badae kutumia kodi na nambari za kumbukumbu kulingana na aina ya kodi au ada anayolipa.
Katika
kulipia kodi ya majengo mlipa kodi atapaswa kutumia nambari ya biashara
(Business Number) 500300, nambari ya biashara kwa ajili ya kulipia kodi
ya mapato – Persona Income Tax ni 600400.
Aidha kwa mteja wa TRA anaetaka kulipia ada ya leseni ya lena - Provisional Driving License nambari ya biashara ni 700500, anaelipia ada ya majaribio ya udereva nambari ya biashara ni 700500.
Mfumo huu wa malipo ya kodi kupitia m-pesa
umehakikiwa vya kutosha kuhakikisha usalama,usiri na uhakika wa huduma
yenye viwango na ubora kwa mlipa kodi hasa kutokana na unyeti wa suala
zima la ulipaji wa kodi lilivyo.
Bagalla
amesema kampuni ya Vodacom ni kampuni inayojali na kuthamini maendeleo
ya Tanzania na watanzania na kwamba kodi ni sehemu muhimu ya mapato kwa
ajili ya maendeleo. Miongoni mwa nguzo muhimu katika nyanja ya
ukusanyaji kodi ni kuwepo na njia rahisi za ukusanyaji kodi na zenye
kutumia gharama nafuu katika ukusanyaji, hivyo basi ni dhahiri m-pesa ni kielelezo cha nguzo hizo.
Huduma ya m-pesa
hadi sasa inawateja zaidi ya milioni sita waliosajiliwa ambao kwa siku
wastani wa shilingi bilioni tatu hupita katika mfumo huu kwa lengo la
kulipia huduma mbalimbali au kutuma fedha miongoni mwa wateja.
Mwisho.
Imetolewa na Ofisi ya Mawasiliano
Vodacom Tanzania
13 June, 2011.
0 comments:
Post a Comment