Sehemu
ya watanzania waishio New York na vitongoji vyake, wakianza kukusanyika
kwa ajili ya kujiandaa kumpokea Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano
wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, kwa ajili ya kukutana na
kuzungumza nao jana Juni 11, 2011.
Idd mtoto wa Kawe jijini Dar es Salaam (kulia) akijumuika na wadau wenzake katika hafla hiyo ya wabongo.
Katika
hafla hiyo hata viongozi wa Jumuiya hiyo hawakuwa nyuma katika
kutekeleza majukumu yao kama kawaida japo ilikuwa ni jumapili, hapa ni
Makamu Mwenyekiti wa Jumuiya hiyo, Miriam Abu (kushoto) na Mweka hazina
msaidizi, Mzee Temba, wakiwa na nyaraka zao ambapo pia walikuwa
wakiendelea na zoezi la kusajiri Watanzania wapya waliokuwa wakitaka
kujiunga na Jumuiya hiyo.
Jumuiya
hiyo ilianza kuwa active zaidi baada ya uchaguzi mkuu wa kuchagua
viongozi wa kuiongoza uliofanyika mwezi April mwaka huu na kuwapata
viongozi wapya kama Mwenyekiti, Haji Hamis na Makamu wake huyo, Katibu
Vicent Mughwai na Katibu msaidizi, Shaban Mseba na Mweka
Hazina, Phillip Lwiza na msaidizi wake, Mzee temba na sasa Jumuiya hiyo
imejipangia majukumu na malengo mengi ikiambatana na mikakati kabambe
ya kuwawezesha kusonga mbele katika kujikwamua kiuchumi na kuweza
kusaidiana kimaisha.
Makamu
wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Mohamed Gharib Bilal na
mkewe Mama Zakhia Bilal Balozi Obeni Sefue na Waziri Juma Duni Haji,
wakisimama na kuimba wimbo wa maalum baada ya kuwasili kwenye eneo la
hafla hiyo.
Makamu
wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Mohammed Gharib Bilal
akiwahutubia Watanzania waishio New York na Vitongoji vyake wakati
alipokutana nao kwa ajili ya mazungumzo nao na kuwatambua ikiwa ni mara
ya kwanza tangu alipoteuliwa kushika nafasi hiyo.
Pichani Juu na Chini; Baadhi
ya Watanzania waishio New York na vitongoji vyake wakimsikiliza kwa
makini Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Mohammed
gharib Bilal alipokuwa akiwahutubia.
Mwenyekiti
wa Jumuiya ya Watanzania waishio New York na vitongoji vyake, Haji
Hamis akizungumza na kutoa utambulisho wa viongozi na wanachama wa
Jumuiya hiyo, ambao hadi sasa wamefiki 110.
Makamu
wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Mohammed Gharib Bilal
na mkewe Mama Zakhia Bilal akiwa katika picha ya pamoja na viongozi wa
jumuiya hiyo baada ya kuwahutubia.
Makamu
wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt Mohammed Gharib Bilal na
mkewe Mama Zakhia Bilal akiwa katika picha ya pamoja na viongozi na
wanachama wa jumuiya.
Makamu
wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Mohammed Gharib Bilal
akisalimia na baadhi ya watanzania hao ikiwa ni sehemu ya kuwaaga baada
ya hotuba yake.
Mke
wa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mama Zakhia Bilal
akipiga picha ya kumbukumbu na baadhi ya kinamama wanachama wa Jumuiya
hiyo.
Makamu wa Rais Dkt. Bilal akipiga picha za kumbukumbu.
Baadhi ya wabongo wakijisevia msosi wakati wa hafla hiyo.
Mchezaji
wa zamani wa timu ya Balimi Fc ya Kagera Henri Rwekagingira (wa pili
kushoto) akipozi na dada zake kwa picha wakati wa hafla hiyo.
Sufianimafoto
pia alikuwa ni miongoni mwa waliohudhuria hafla hiyo hapa akipozi na
mchezaji wa zamani wa timu ya Balimi Fc ya Kagera Henri (wa pili
kushoto) na dada zake.
(Picha Zote na Muhidin Sufiani-OMR).
0 comments:
Post a Comment