Bunge Lapitisha Mswada Muhimu
Ugiriki
Makabiliano
makali kati ya polisi na waandamanaji wanaopinga mpango wa kuunusuru uchumi wa
Ugiriki yameendelea mjini Athens kutwa nzima.
Raia
wanapinga mpango huo ambapo kodi itaongezeka maradufu
Mabomu
yaliotengenezwa na petroli yamekua yakilipukua jioni nzima, huku polisi
wakutuliza ghasia wakiwarushia watu hao waliokusanyika nje ya jengo la bunge
gesi za kutoa machozi.
Lakini
licha ya vurugu hizo, mswada wa serikali uliochochea machungu haya yote
ulipitishwa japo katika mazingira ya ushindani mkali.
Wabunge
155 waliunga mkono pendekezo hilo huku wengine 138 wakipinga. Leo wabunge
watapiga kura tena kubadilisha sheria ili mpango huo utekelezwe.
Waziri
mkuu George Papandreou amelenga kubana matumizi ya serikali ili ifikiapo mwaka
wa 2015 watakuwa na hazina ya pauni bilioni 25.
Pamoja
na hilo, amependekeza kupandisha kodi ili kuongezea kipato cha serikali, hatua
iliochochea maandamano hayo nchini humo.
Lakini
waziri mkuu Papandreou anasema mpango huo ukitibuka ni sawa na kuangamiza nchi
hiyo.
Umoja
wa ulaya umepongeza bunge kupitisha pendekezo hilo ambapo liki zingatiwa
serikali ya Ugiri huenda ikafaulu kulipa malimbikizi ya madeni yake.
Hata
hivyo bado kuna wale ambao hawaamini kuwa mpango huo utafaulu.
Serikali
ya Ugiriki sasa inatarajia kupata mkopo wa euro billioni 110 kutoka kwa shirika
la fedha duniani na umoja wa ulaya kutatua matatizo yake ya kiuchumi.
0 comments:
Post a Comment