Connor Wickham
Wickham, mwenye umri wa
miaka 18, anaweza kuwa mchezaji wa Sunderland katika muda wa saa 24, iwapo
watakubaliana juu ya masuala binafsi pamoja na kukamilisha uchunguzi wa kiafya.
Kandarasi hiyo ya mchezaji wa timu ya
taifa ya England ya vijana wasiozidi miaka 21, ambaye alianza kuchezea Ipswich
akiwa na miaka 16, huenda ikafika kiwango cha pauni za Uingereza milioni £12.5m.
Awali ilidhaniwa angejiunga na timu
ya Tottenham au Liverpool.
Haikufahamika mustakabali wake kwenye
timu hiyo ungekuwaje, licha ya kuongeza kandarasi yake na Ipswich hadi mwezi
Aprili 2014.
Historia fupi
Wickham alijumuishwa kwenye timu ya
England ya wachezaji wasiozidi umri wa miaka 21 kwa michuano ya bara Ulaya
lakini hakucheza mechi hata moja.
Tangu kujiunga na Ipswich mwezi Julai
2008 amechezea kikosi cha kwanza mara 37 na kuingia kama mchezaji wa akiba mara
35,kwa jumla akifunga magoli 15.
Mwezi wa Mei 2010 Wickham alisaidia
England kupata ushindi kwenye michuano ya bara Ulaya ya vijana wasiozidi miaka
17, baada ya kufunga bao la ushindi. Katika fainali hiyo England iliifunga
Uhispania 2-1.
Kocha wa Ipswich Paul Jewell alisema
wiki iliopita kwamba alitarajia timu nyingi kuonyesha nia ya kumsajili Wickham
lakini wao hawakuwa na haraka ya kumuuza mshambulizi huyo.
0 comments:
Post a Comment