Mgeni
rasmi Mkurugenzi wa Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Prof.
Mwansoko akizungumza kwa niaba ya Naibu Waziri wa Wizara hiyo Dkt. Fenela
Mkangara wakati wa uzinduzi wa FLAVIANA MATATA FOUNDATION ambapo alimpongeza
kwa kuonyesha kujali maendeleo ya mtoto wa kike hapa nchini na kuahidi
kushirikiana naye bega kwa bega.
Mwanamitindo
Flaviana Matata anayefanya kazi zake za uanamitindo katika jiji la New York
nchini Marekani akizungumza machache wakati wa uzinduzi wa Taasisi yake
inayoitwa FLAVIANA MATATA FOUNDATION itakayokuwa ikisaidia na kusomesha watoto
wa kike wasiokuwa na wazazi au walezi (Yatima).
Taasisi
hiyo ambayo itakuwa ikifanya kazi kwa ukaribu na wadau mbalimbali ambao
wamekuwa wakisaidia jamii hapa nchini akiwemo Mbunge wa Singida Mjini Mh.
Mohammed Dewji, Mwamvita Makamba pamoja na wadau wengine. Uzinduzi huo
umefanyika katika hoteli ya Kilimanjaro Kempinski na kuhudhuriwa na watu
mbalimbali maarufu wakiwamo Wabunge, Wafanyabiashara wakubwa pamoja na Viongozi
wa Serikali.
Ofisa
Mtendaji Mkuu wa Masoko na Mahusiano wa Vodacom Tanzania Mwamvita Makamba
akieleza nia ya Flaviana Matata kuzindua Taasisi hiyo. Mwamvita Makamba ni
mmoja wa wadau watakaokuwa wakisimamia taasisi hiyo pamoja wakishirikiana
na Mkurugenzi wa Utafiti na Maendeleo wa Clouds FM Ruge
Mutahaba.
0 comments:
Post a Comment