Mkurugenzi
Mkuu wa Bodi ya Biashara ya Nje Ramdhan Hashim Khalfan akizungumzia
maandalizi ya Maonyesho ya 35 ya Kimataifa ya Biashara ya Dar es Salaam
ambapo amesema yapo katika hatua za mwisho na kuwataka wananchi
kujitokeza kwa wingi siku ya uzinduzi rasmi tarehe 28 Juni, 2011.
Mkurugenzi
Mkuu wa Bodi ya Biashara ya Nje Ramdhan Hashim Khalfan akionyesha
hatua za mwisho za ukarabati wa lango la kuingilia katika uwanja wa
maonyesho ya Saba Saba ambapo amesema kwa mwaka huu siku uzinduzi
Viingilio vitakuwa Sh. 3000 (wakubwa) na Sh. 1000 (watoto) wakati katika
siku za kawaida za maonyesho hayo ni sh.2500 (wakubwa) na Sh.500
(watoto).
Kaimu
Mkurugenzi Ukuzaji Masoko na Huduma Masha Hussein akionyesha waandishi
wa habari moja ya mahema yatakayotumiwa na wafanya biashara katika
maonyesho hayo ambapo amesema hema moja lina ukubwa wa Mita Mraba 1000
na uwezo wa kuingiza washiriki 60. Kushoto ni Afisa Mwandamizi Biashara
za Nje Bw. Stephen Kobero.
Hema Kuu kutakapofanyikia uzinduzi rasmi wa maonyesho hayo.
Bustani
iliyotengenezwa kitaalam kwa maua yaliyoandika maonyesho ya 35 ya
Kimataifa ya Biashara ya Dar es Salaam iliyopo nje ya uwanja huo.
(Picha
na Geofrey Mwakibete wa Mo Blog).
0 comments:
Post a Comment