SONYA_FLAWLESS_IMG
WE CREATE GREATNESS. | Professional Networker | Global Business Builder | Health And Wellness Coach | YOUR DREAM OUR PLAN.

Friday, June 17, 2011

UMOJA WA AFRIKA WAIONYA UMOJA WA MATAIFA JUU YA SUALA LA LIBYA

Hatari tupu Libya.

Waasi wa Libya wamedhibiti miji mitatu iliyo kwenye barabara inayoelekea mji mkuu wa Libya, Tripoli.
Miji hiyo mitatu ipo katika njia panda muhimu, inayounganisha maeneo mbali mbali magharibi mwa Libya.
Nazo ndege za NATO pia zimeshambulia tena eneo lenye makazi ya kiongozi wa Libya Muammar Gaddafi.
Wakati huo huo, Umoja wa Mataifa umeonywa na Umoja wa Afrika kuwa operesheni ya kijeshi nchini Libya, imeanzisha “mfano wa hatari.”
Umoja huo wa Afrika umetoa wito wa kusitishwa kwa mapigano ili zitafutwe njia za kusaidia kupatikana kwa ufumbuzi wa tatizo hilo.

0 comments:

Post a Comment