SONYA_FLAWLESS_IMG
WE CREATE GREATNESS. | Professional Networker | Global Business Builder | Health And Wellness Coach | YOUR DREAM OUR PLAN.

Thursday, May 5, 2011

BENKI YA KCB TANZANIA YATOA MSAADA KWA WATOTO YATIMA

Mkuu wa Kitengo cha Masoko na Mahusiano wa KCB Tanzania Christine Manyenye akimkabidhi mtoto Beatrice Phinius wa kituo cha watoto yatima Amani Orphanage Centre cha Boko moja ya misaada iliyotolewa na wafanyakazi wa benki hiyo kwa ajili ya watoto wa kituo hicho. Anayeshuhudia katikati ni Mkurugenzi wa kituo hicho Margaret Mwegalawa.
Mkuu wa Kitengo cha Masoko na Mahusiano wa KCB Tanzania Christine Manyenye na mfanyakazi wa benki hiyo tawi la Samora, Shose Kombe wakiwa wamewabeba watoto yatima wanaolelewa na  Kituo cha watoto yatima cha Amani Orphanage Centre cha Boko jijini wakati wa hafla ya kukabidhi msaada wa vyakula wenye thamani ya milioni 1.5/-.
Mkuu wa Kitengo cha Masoko na Mahusiano wa KCB Tanzania Christine Manyenye (Kushoto) akiteta jambo na Afisa Mahusiano kwa Umma wa benki hiyo Gigi Maajah mara baada ya kukamilika kwa hafla ya kukabidhi msaada kwa Kituo cha watoto yatima cha Amani Orphanage Centre cha Boko jijini Dar es Salaam.
Baadhi ya misaada iliyotolewa na KCB TANZANIA kwa kituo cha watoto yatima cha Amani Orphanage Centre cha Boko jijini Dar es Salaam. Benki hiyo ilikabidhi mchele, sukari, Unga wa Sembe, nguo za aina mbalimbali zikiwemo shuka za kujifunika na kitanda cha mtoto mdogo vyote vikiwa na thamani ya shilingi milioni 1.5/-.
Mkuu wa Kitengo cha Masoko na Mahusiano wa KCB Tanzania Christine Manyenye akimkabidhi mtoto Jack Saguno wa kituo cha watoto yatima Amani Orphanage Centre cha Boko moja ya misaada iliyotolewa na wafanyakazi wa benki hiyo kwa ajili ya watoto wa kituo hicho. Anayeshuhudia katikati ni Mkurugenzi wa kituo hicho Margaret Mwegalawa.
Watoto yatima wa kituo cha Amani Orphanage Centre cha Boko jijini wakimsikiliza Mkuu wa Kitengo cha Masoko na Mahusiano wa KCB Tanzania Christine Manyenye (hayupo pichani) wakati wa hafla ya kukabidhi msaada uliotolewa na wafanyakazi wa benki hiyo wenye thamani ya milioni 1.5 kwa watoto 60 wanaolelewa kituoni hapo.
Habari zaidi:

0 comments:

Post a Comment