SONYA_FLAWLESS_IMG
WE CREATE GREATNESS. | Professional Networker | Global Business Builder | Health And Wellness Coach | YOUR DREAM OUR PLAN.

Wednesday, September 22, 2010

Poulsen awapeleka Ulaya Ngassa, Mgosi


Kocha Mkuu wa Taifa Stars, Jan Poulsen.
Na Wilbert Molandi
KOCHA Mkuu wa Taifa Stars, Jan Poulsen amesema kama Andries Iniesta na Lionel Messi wanaweza kucheza vyema soka la kimataifa, hakuna kitachowazuia Mrisho Ngassa na Mussa Hassan Mgosi kusakata kabumbu Ulaya licha ya maumbile yao kuwa madogo.
Akizungumza na Championi Jumatano, Poulsen raia wa Denmark alisema, vimo vidogo walivyonavyo Ngassa na Mgosi visiwakatishe tamaa ya kutokwenda kucheza soka la kulipwa badala yake waongeze bidii ya mazoezi yatakayowawezesha kupiga hatua nyingine kutokana na uwezo wao kuruhusu kucheza nje ya nchi.
Iniesta na Messi wote ni viungo washambuliaji wanaocheza kwa mafanikio katika klabu ya Barcelona ya Hispania licha ya kuwa wafupi kama ilivyo kwa Ngassa anayecheza Azam FC na Mgosi wa Simba ambao wamo katika kikosi cha Stars. 
“Tazama wachezaji kama Andries Iniesta na Lionel Messi, ni kati wachezaji wenye maumbile madogo angalia uwezo wao ulivyo wakiwa uwanjani na ndiyo kama walivyo Ngassa na Mgosi, naamini watacheza soka la kulipwa waongeze bidii zaidi. 
“Nimefurahishwa na uwezo wa Ngassa na Mgosi ambao nimewaona tangu nilipofika, wana sifa ya kucheza nje ya nchi. Vimo walivyonavyo siyo sababu ya kukosa nafasi ya kucheza kutokana na kuwepo nyota wengi wanaocheza Ulaya kuwa maumbile kama wao.
“Kocha wa timu siku zote haangalii umbile la mchezaji bali uwezo wake uwanjani, unaweza ukawa na mchezaji mrefu lakini kiwango chake kikawa kidogo na akazidiwa na mwenye umbile dogo,” alisema Poulsen mwenye umri wa miaka 64.

0 comments:

Post a Comment