SONYA_FLAWLESS_IMG
WE CREATE GREATNESS. | Professional Networker | Global Business Builder | Health And Wellness Coach | YOUR DREAM OUR PLAN.

Wednesday, September 22, 2010

Azma ya Rais Museveni ya kutetea wadhifa wake mwaka ujao yapingwa kortini

Sample Image
Afisa wa zamani wa ngazi za juu katika jeshi la Uganda amekwenda mahakamani kupinga azma ya Rais Yoweri Museveni wa nchi hiyo ya kutetea wadhifa wake kwenye uchaguzi mkuu wa mwaka ujao. Maguru Ruhinda ameitaka mahakama kuu ya Uganda kubatilisha uteuzi wa Museveni kuwa mgombea urais kwa tikiti ya chama tawala cha NRM kwa madai kuwa chama hicho kilimzuia asimpinge Rais Museveni kwenye uchaguzi wa chama mwezi uliopita. Ruhinda pia ameitaka mahakama imchukulie hatua za kisheria katibu mkuu wa NRM Amama Mbabazi kwa kumzuia kugombea uongozi wa chama hicho. Rais Museveni ambaye amekua uongozini tangu mwaka 1986 anatetea wadhifa wake huku akiwa Rais aliyetawala kwa muda mrefu zaidi katika eneo la Afrika Mashariki. 

0 comments:

Post a Comment