SONYA_FLAWLESS_IMG
WE CREATE GREATNESS. | Professional Networker | Global Business Builder | Health And Wellness Coach | YOUR DREAM OUR PLAN.

Tuesday, July 13, 2010

Uchunguzi mpya wa maoni waonyesha umaarufu wa Rais Obama unazidi kupungua
Sample ImageUchunguzi mpya wa maoni uliofanywa na gazeti mashuhuri la The Washington Post kwa ushirikiano na kanali ya televisheni ya ABC nchini Marekani umeonyesha kuwa umaarufu wa Rais Barack Obama wa nchi hiyo umepungua kwa kiwango kikubwa. Matokeo ya uchunguzi huo yanaonyesha kuwa takriban asilimia 60 ya Wamarekani hawana imani na Rais Obama hususan katika upande wa kufanya maamuzi muhimu yanayoiathiri nchi yao. Weledi wa masuala ya kisiasa wamesema kuwa kushindwa stratejia za Washington huko Afghanistan na Iraq na suala la kuvuja mafuta ya petroli katika ghuba ya Mexico ambapo Marekani hadi sasa haijafanikiwa kulitatua tatizo hilo ni miongoni mwa mambo yaliyopelekea kiongozi huyo apoteze zaidi umaarufu wake. Mwaka mmoja uliopita Rais Obama alikuwa miongoni mwa viongozi mashuhuri zaidi duniani lakini hali hiyo imekua ikibadilika kila uchao.

*******************
Mwakwere ahifadhi kiti chake cha ubunge kwenye uchaguzi mdogo wa Matuga nchini Kenya
Sample Image 










Ali Chirau Mwakwere amefanikiwa kukihifadhi kiti chake cha ubunge kwenye uchaguzi mdogo wa eneo bunge la Matuga. Mwakwere ambaye anatoka katika chama cha PNU kinachoongozwa na Rais Mwai Kibaki, amepata kura 16,350 na hivyo kumshinda mpinzani wake wa karibu Hassan Mwanyoha kutoka chama cha ODM kinachoongozwa na Waziri Mkuu Raila Odinga aliyepata kura 10,887. Ali Chirau Mwakwere Waziri wa zamani wa Uchukuzi alivuliwa ubunge na mahakama moja ya Mombasa kufuatia kesi iliyokuwa imewasilishwa mahakamani kupinga kuchaguliwa kwake wakati wa uchaguzi mkuu wa mwaka 2007 kwa madai kuwa aliiba kura kwenye uchaguzi huo. Nafasi ya Uwaziri aliyokuwa akishikilia hadi alipovuliwa ubunge hadi sasa haijapewa mtu mwengine na inatarajiwa kuwa atarejeshewa wadhifa huo na Rais Kibaki baada ya kuapishwa upya bungeni.

0 comments:

Post a Comment