SONYA_FLAWLESS_IMG
WE CREATE GREATNESS. | Professional Networker | Global Business Builder | Health And Wellness Coach | YOUR DREAM OUR PLAN.

Tuesday, July 13, 2010


ICC - Hati ya pili ya kukamatwa Bashir

Rais Omar Al Bashir wa Sudan
Mahakama ya uhalifu wa kivita ya ICC imetoa hati ya pili ya kukamatwa kwa rais wa Sudan Omar Hassan Al Bashir. Hati hiyo imetolewa kwa kosa la pili la mauaji ya kimbari.
Kiongozi wa mashtaka mwandamizi wa mahakama hiyo Louise Moreno Ocampo amemlaumu Bashir kwa kuhusika katika kuchochea mauaji ya makabila matatu mjini Darfur kusini mwa Sudan.
Hati ya awali kutoka kwa mahakama hiyo iliyotolewa mwezi Machi mwaka uliopita ilimwekea Bashiri mashtaka ya uhalifu wa kivita.
Hata hivyo mshirika mkuu wa Rais Bashir Rabie Abdelatif ametaja shtaka hilo kama upuzi mtupu.
Marekani ilitoa wito kwa rais Bashir ajiwasilishe kwa mahakama hiyo ya ICC kujibu mashtaka yanayomkabili.
Zaidi ya watu 3,000 wanadaiwa kuuawa katika eneo la Dar Fur tangu mapigano kuzuka mwaka wa 2003.
***************************
Maaskofu wanawake waruhusiwa - Uingereza

Askofu mwanamke wa kanisa Anglikana
Kanisa la Kianglikana nchini Uingereza limechukua hatua kuwaruhusu wanawake kuhudumu kama maaskofu licha ya onyo kutoka kwa viongozi wao wenye itikadi kali kuwa watajiondoa kutoka kwa kanisa hilo.
Viongozi hao wamesema kuwa hatua hiyo inaenda kinyume na mafundisho ya bibilia yanayokataza wanawake kuwa maaskofu.
Hata hivyo baraza kuu la kanisa hilo, Synod, limekanusha hilo na kupania kuwapa wanawake haki sawa na wanaume katika uongozi wa kanisa.
Kiongozi wa kanisa hilo, askofu mkuu wa Canterbury Rowan Williams amekiri kuwa kuna changa moto kuu la kushikilia kanisa pamoja kwani migawanyiko imekithiri katika kanisa hilo.

Askofu Williams
Suala hilo limezua utata miongoni mwa jamii nzima ya kianglikana kote duniani.
bbc swahili

0 comments:

Post a Comment