SONYA_FLAWLESS_IMG
WE CREATE GREATNESS. | Professional Networker | Global Business Builder | Health And Wellness Coach | YOUR DREAM OUR PLAN.

Wednesday, June 9, 2010

Mdau aliyemkumbatia Ricardo Kaka National Stadium apata dhamana

Huyu ndie kijana aliyewashangaza watanzania baada ya kuruka senyenge za uwanja wa Taifa na kuingia uwanjani kwenda kumpiga Hug mchezaji wa Brazil KAKA . watu walishangaa sana kwani haikujilikana kwa hafla jama katokea kwa wapi. hafla yupo uwanjani wakati bado soka inaendelea kupigwa ..Yeye alitaka kumpa Hug kaka tu basi ili atimize ndoto zake. Kijana Nagari Kombo (kushoto), akisindikizwa na askari kanzu, wakitoka Kituo Kikuu Polisi (Police Centre), Dar es Salaam jana mara baada ya Kamanda wa Polisi, Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Suleiman Kova, kutangaza kumpatia dhamana na suala lake kupelekwa Shirikisho la Mpira wa Miguu nchini (TFF) na Kamati ya Uendeshaji na Usimamizi wa Uwanja wa Taifa kwa ajili kushughulikiwa kwa sheria zinazotawala mambo ya michezo. Kwa mujibu wa Afande SKova, Kombo atakuwa nje kwa dhamana huku akitakiwa kuripoti mara moja kila wiki katika kituo hicho wakati suala lake likishughulikiwa.
.
Kombo akiwa kwenye gari na babake (kulia) pamoja na Askari kanzu wakielekea Polisi Chang'ombe kupewa dhamana.

michuzi blog

0 comments:

Post a Comment