
Jumuiya ya Wafanyabiashara wa Kariakoo wameahidi kuendelea kutafuta suluhu kwa njia ya mazungumzo na serikali juu ya mgogoro wa makontena ambayo yamezuiliwa bandarini, kitendo ambacho kimeathiri biashara zao kwa mda mrefu sasa kwani wemeshindwa kufanya biashara ndani na nchi jirani kwa takriban zaidi ya wiki tatu.
Tamko hili lililotolewa na Jumuiya Hii wiki iliopita, limeeleza kuwa tayari wametuma maombi kwa wizara husika na idara za serikali za mapato ili kuwepo na mkutano utakaoweza kutizama jinsi ya kutatua mgogoro wa makontena zaidi ya 400 ambayo yamezuiliwa bandarini.



