SONYA_FLAWLESS_IMG
WE CREATE GREATNESS. | Professional Networker | Global Business Builder | Health And Wellness Coach | YOUR DREAM OUR PLAN.

Monday, February 17, 2014

LULU APANDISHWA KIZIMBANI TENA, KESI YAKE YAAHIRISHWA....

Staa wa filamu za Kibongo, Elizabeth Michael 'Lulu' pamoja na Mahsein Awadh 'Dk. Cheni' wakipitia Gazeti la Ijumaa Wikienda ndani ya Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam wakati wakisubiri kusikiliza kesi inayomkabili Lulu juu ya kifo cha msanii Steven Kanumba. 
Leo February 17 kutoka Mhakama kuu kanda ya Dar es salaam,msanii wa maigizo nchini Tanzania Elizabeth Michael maarufu Lulu alikuwa akisomewa shitaka lake la kuua bila kukusudia msanii mwenzake wa maigizo Steven Kanumba April 07 2012  eneo la Vatican.
Akisoma maelezo ya awali wakili wa serikali Monica Mbogo mbele ya Jaji anayesikiliza kesi hiyo Rose Teemba amesema mshtakiwa siku ya tukio kulikuwa na ugomvi kati ya marehemu na mshtakiwa na baadaye mshtakiwa aliondoka usiku wa saa sita baada ya marehemu kuanguka chumbani ambapo alfajiri ya february 07  majira ya saa 11 alfajiri Lulu alikamatwa eneo la Bamaga.
Kwa upande wake wakili  Peter Kibatala ambaye anamtetea Lulu amesema wameridhishwa na sehemu kubwa ya  maelezo ya awali ya mteja wao, ambapo kesi hiyo imeahirishwa mpaka itakapopangwa tena huku kila upande ukitarajia kuleta madhahdi watatu.
1
Baadhi ya wasanii wa Bongo Movie waliohudhuria leo mahakamani ni Dr.Cheni na Kajala.
4
6
7
Elizabeth Michael 'Lulu' (katikati) akiwa na mama yake mzazi, Lucresia Karugila (wa pili kushoto) na Dk. Cheni (kulia) ndani ya Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam leo.
CREDIT. MILLARD AYO NA GPL

0 comments:

Post a Comment