SONYA_FLAWLESS_IMG
WE CREATE GREATNESS. | Professional Networker | Global Business Builder | Health And Wellness Coach | YOUR DREAM OUR PLAN.

Sunday, October 27, 2013

Tanzanite Ilivyong'ara Baada YaKuirarua Mozambique Mabao 10 - 0

 

 Kikosi cha timu ya soka ya wanawake ya Tanzanite kikiwa katika picha ya pamoja,kabla ya kuanza kwa mchezo wao dhidi ya Mozambique uliopigwa jana jioni kwenye uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.Hadi mwisho wa mchezo,Tanzanite iliibuka kidedea kwa ushindi mnono wa mabao 10 - 0.
 
 Waamuzi wa mchezo huo.

 Kikosi cha Mozambique.
 
Raha ya ushindi.
PICHA NA ANKAL MICHUZI

Timu ya soka ya taifa ya wanawake kwa vijana chini ya umri wa miaka 20, The Tanzanites imeifunga Msumbiji mabao 10-0 katika mechi ya kwanza ya raundi ya Kwanza ya Kombe la Dunia katika Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam jioni ya leo.
Mchezo huo uliohudhuria na mashabiki wachache mno, hadi mapumziko tayari Tanzanites walikuwa mbele kwa mabao 5-0.
Majina ya wapachika magoli na muda waliopachika mabao hayo, upo kwenye mabano kama ifuatavyo:-
Neema Paul (dk 6)Shelder Boniface (dk 24 na 80)Deonesia Daniel (dk 32, dk 86 kwa penati)Amina Ali (dk 41, 82 na dk 89)Neema Paul Stumai Abdallah (dk 90)
Kocha wa The Tanzanites: Rogasian Kaijage
Kikosi cha Tanzania: Celina Julius, Stumai Abdallah, Maimuna Said/Amina Hebron dk60, Fatuma Issa, Anastazia Anthony, Deonisia Daniel, Vumilia Maarifa, Amina Ali, Neema Paul, Shlder Boniface na Theresa Yona.
Kikosi cha Msumbiji: Paulina Jambo/Catarina Francue dk50, Esperanca Malaita/Delice Assane dk52, Felismisa Moiane, Emma Paulino, Gilda Macamo, Deolinda Gove, Jessica Zunguene, Cidalia Cuta, Nelia Magate, LonicaTsanwane na Onesema David.

NEWS: WAVUTI
 

0 comments:

Post a Comment