SONYA_FLAWLESS_IMG
WE CREATE GREATNESS. | Professional Networker | Global Business Builder | Health And Wellness Coach | YOUR DREAM OUR PLAN.

Wednesday, February 5, 2014

ZAIDI YA KILO 200 ZA MADAWA YA KULEVYA AINA YA HEROIN ZAKAMATWA BAHARI YA HINDI


Jahazi lililokamatwa na madawa ya kulevya.

Polisi wa Kikosi cha Kupambana na Dawa za Kulevya wakifungua dawa zilizokamatwa jana kwenye jahazi liitwalo Kunarak-Iran lililokutwa katika Bahari ya Hindi eneo la Tanzania likiwa na kilo 201 za heroini, pamoja na raia wanane wa Iran na  Wapakistan wanne. Picha na Michael Jamson 

ZAIDI ya kilo 200 za madawa ya kulevya aina ya Heroin yamekamatwa na kikosi cha polisi wanamaji katika Bahari ya Hindi yakisafirishwa kutokea nchini Irani pamoja na mabaharia kumi na wawili kutoka nchi ya Irani na Pakistani.
Kamanda wa polisi kikosi cha wanamaji Mboje Kanga ameeleza kuwa tukio hilo lililotokea usiku wa tarehe 4 majira ya saa sita usiku ambapo waliweza kukamata jahazi hilo na mabaharia kumi na mbili wote wakiwa hawaijui lugha ya Kiswahili wala Kingereza na jahazi lao halikuwa na utambulisho wowote wa sheria za majini.
Mkuu wa kitengo cha kudhibiti dawa za kulevya, Godfrey Nzowa amesema jahazi hilo liliweza kukamatwa baada ya kikosi cha polisi cha wanamaji kuendelea na operesheni zake za doria majini na mara baada ya kulitilia shaka waliweza kulikamata na baada ya kulikagua walikamata shehena hiyo ya madawa ya kulevya aliyoyataja kuwa ni aina ya Heroin ambayo mengi huzalishwa nchini.
Chanzo: ITV

0 comments:

Post a Comment