Wawakilishi
wa Tanzania bara kwenye mashindano ya klabu Bingwa barani Afrika timu
ya Young Africans itashuka dimbani siku ya jumamosi kuivaa timu ya
Komorozine de Domoni ya Visiwa vya Comoro katika mchezo wa hatua ya
awali ya Klabu Bingwa barani Afrika.
Young Africans itashukda dimbani kuhakikisha inaendeleza wimbi la
ushindi kufuatia kupata ushindi katika mchezo wa mwisho dhidi ya timu ya
Mbeya City mchezo ambao ulikuwa ni kuwasisimua kwa wapenzi wa soka
nchini kwa ujumla.
Kikosi cha Young Africans chenye wachezaji 25 kimeweka kambi mjini
Bagamoyo kujiandaa na mchezo huo ambapo wachezaji wake wote wapo katika
hali nzuri na wakiendelea na maandalizi ya mchezo huo.
Kocha Mkuu wa
Young Africans mholanzi Hans Van der Pluijm jana amekifanyisha kikosi
chake mazoezi mara mbili asubuhi na jioni , huku leo akitarajia
kuendelea na mazoezi jioni katika kuwaweka sawa kwa ajii ya mehci hiyo
ya jumamosi.
Akiongelea mchezo wa jumamosi kocha Hans alisema anashukuru vijana
wake wote wako fit, hakuna majeruhi hata mmoja na kikubwa wakiwa mjini
Bagamoyo wanapata muda wa kupumzika mara baada ya mazoezi jambo ambalo
kiafya ni muhimu.
Viingilio vya mchezo huo wa jumamosi ni:
VIP A Tshs 30,000/=
VIP B & C Tshs 20,000/=
Orange Tshs 10,000/=
Blue & Green Tshs 5,000/=
Aidha tiketi zitaanza kuuzwa siku moja kabla ya mechi (ijumaa) katika vituo vifuatavyo:
Makao Makuu - Young Africans SC
Kariakoo - Sokoni
Shule ya Sekondari Benjamini - Uhuru
Mwenge - Stand
Oil Com - Ubungo
Steers - Mtaa wa Samora
Dar Live - Mbagala
Oil Com - Buguruni
Uwanja wa Uhuru - Chang'ombe
Kimara Mwisho - Stand
0 comments:
Post a Comment