MBUNGE
wa Jimbo la Iringa Mjini, Mchungaji Peter Msigwa (48) leo amefikishwa
katika mahakama ya hakimu mkazi Iringa akituhumiwa kwa kosa la kujeruhi
katika kampeni za uchaguzi mdogo wa udiwani kata ya Nduli.Kama anavyoonekana hapa kiwasalimu wafuasi wake mahakamani hapo
MBUNGE
wa Jimbo la Iringa Mjini, Mchungaji Peter Msigwa (48)akiwa ndani ya mahakama
MBUNGE
wa Jimbo la Iringa Mjini, Mchungaji Peter Msigwa (48)akiteta na wakili wake Lwezaula Kaijage
Chiku Abwao (MB) baada ya kumdhamini akitoka katika mahakama hiyo
Akisalimia wafuasi wake baada ya kutoka mahakamani kwa dhamana
---
Na Francis Godwin Blog,Iringa
MBUNGE
wa Jimbo la Iringa Mjini, Mchungaji Peter Msigwa (48) leo amefikishwa
katika mahakama ya hakimu mkazi Iringa akituhumiwa kwa kosa la kujeruhi
katika kampeni za uchaguzi mdogo wa udiwani kata ya Nduli.
Mbele
ya Hakimu Mkazi wa Mahakama ya Wilaya ya Iringa, Godfrey Isaya,
Mwendesha Mashtaka wa Polisi, Elizabeth Swai alisema Mchungaji Msigwa
alitenda kosa hilo Febrauri 5, 2014 katika kijiji cha Nduli, mjini
Iringa.
Alisema
Mchungaji Msigwa anashitakiwa kwa kumjeruhi Salum Kahita kinyume na
kifungu kidogo namba 225 cha sheria ya kanuni za adhabu.
Akiwa
amefunguliwa kesi ya jinai namba 28 ya mwaka 2014, Mchungaji Msigwa
anayetetewa na wakili Lwezaula Kaijage alikana kosa hilo na hakimu
aliahirisha kesi hiyo itakayotajwa tena Machi 10, mwaka huu kwa kile
kilichoelezwa kwamba uchunguzi wake haujakamilika.
Pamoja
na Mchungaji Msigwa, jeshi la Polisi limewapandisha kizimbani Meshack
Chonanga (22) na Paulo Mapunda wote wakazi wa kijiji cha Nduli mjini
Iringa wakituhumiwa kumjeruhi Alex Mpiluka wakati wa kampeni hizo.
Watuhumiwa hao walirudisha mahabusu ya mahakama hiyo baada ya wadhamini wao kuchelewa kufika mahakamani hapo.
Kama
ilivyokuwa kwa Mchungaji Msigwa, nao kila mmoja anatakiwa kuwa na
wadhamini wawili watakaoweka dhamana ya ahadi ya Sh Milioni 2.
0 comments:
Post a Comment