Emmanuel
Okwi ambae ni mshambuliaji wa kimataifa wa Uganda aliyesajiliwa na
klabu ya Yanga, ameruhusiwa rasmi kikiwa ni kibali kutoka shirikisho la
soka duniani (FIFA) kushiriki kuichezea timu yake ya sasa ambayo ni
Yanga.
Okwi ambaye alikuwa amesimamishwa kutokana suala la mgogoro mauzo
yake uliokuwa ukizihusisha timu zake za zamani Simba SC ya Tanzania na
Etoile Du Sahel ya Tunisia, sasa ameruhusiwa kuitumikia Yanga huku FIFA
ikiendelea kufuatilia kiundani kuhusu deni la Simba la dola 300,000
wanaloidai Etoile.
Fedha hiyo ilikuwa ya uhamisho wa mchezaji huyu kutoka Simba kwenda
Tunisia takribani miaka miwili iliyopita ambapo baada ya kupata
greenlight, Okwi sasa ataweza kuitumikia Yanga katika michuano ya ligi
kuu na kombe la klabu bingwa ya Afrika.
NA MIRLADAYO.COM
0 comments:
Post a Comment