Abiria mmoja alinusurika ajali hiyo
iliyohusisha ndege aina ya Hercules C-130 iliyoanguka katika eneo la
milima ya Oum al-Bouaghi, ikiwa njiani kuelekea mji wa Constantine.
Rais wa nchi hiyo Abdelaziz Bouteflika amewasifu wanajeshi waliopoteza maisha yao na kuwataja kama wafia dini wa taifa hilo.Ripoti zinasema hali mbaya ya anga ilisababisha ajali hiyo ya ndege.
Wengi wa abiria sabini na nane waliokuwa ndani ya ndege hiyo ni maafisa wa kijeshi na familia zao.
Mwanajeshi aliyenusurika, anaripotiwa kuendelea kupokea matibabu katika
hospitali moja mjini Constantine baada ya kupata majeraha ya kichwa.
Wizara ya Ulinzi imesema kuwa imeunda tume maalum kuchunguza ajali hiyo
na kuwa Ahmed Gaid Salah, ambaye ni mkuu wa majeshi na naibu waziri wa
Ulinzi atazuru eneo la ajali hiyo.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotumwa kwa vyombo vya habari, wizara ya ulinzi
imesema kuwa hali mbaya ya anga iliyohusisha kimbunga na mvua kubwa ya
barafu ilisababisha ajali hiyo.
Runinga ya taifa ilionyesha picha za ajali hiyo.
Awali maafisa wa Ulinzi na shirika hilo la habari waliripoti kuwa watu
103 walikuwa ndani ya ndege hiyo lakini idadi hiyo ilipunguzwa hadi watu
sabini na nane
BBC SWAHILI..
0 comments:
Post a Comment