SONYA_FLAWLESS_IMG
WE CREATE GREATNESS. | Professional Networker | Global Business Builder | Health And Wellness Coach | YOUR DREAM OUR PLAN.

Wednesday, December 25, 2013

Kutoka Gazeti la Mwananchi:Emmanuel Nchimbi ,Shamsi Vuai Nahodha Bado Wanaweza kuwania urais

Emmanuel Nchimbi
Shamsi Vuai Nahodha
------
 Baadhi ya wasomi nchini wamesema kwamba licha ya hatua iliyochukuliwa na Rais Jakaya Kikwete kutengua uteuzi wa mawaziri wanne, kugusa mustakabali wa kuwania urais wa miongoni mwa wanasiasa hao katika Uchaguzi Mkuu wa 2015, wanaweza kuwania nafasi hiyo kwa kuwa waliwajibika kisiasa.

Mawaziri walioenguliwa kutokana na athari za Operesheni Tokomeza Ujangili ni wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Dk Emmanuel Nchimbi, Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi, Dk Mathayo David, Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Shamsi Vuai Nahodha na Waziri wa Maliasili na Utalii, Balozi Khamis Kagasheki.

Wakati Nchimbi akitajwa kuwa mmoja wa wanasiasa tishio katika mbio za kuwania urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM) katika uchaguzi mkuu ujao, Nahodha anatajwa kuwa mmoja wa wale watakoingia katika kinyang’anyiro cha nafasi hiyo upande wa Zanzibar lakini baada ya Dk Shein kumaliza muda wake wa vipindi viwili.

Katika msingi huo, gazeti hili liliarifiwa kuwa baada ya tangazo la kutenguliwa kwa uwaziri wao, baadhi ya kambi zinazojiwinda kwa ajili ya kuwania nafasi za juu za uongozi wa nchi 2015, zilishangilia na kuandaa tafrija za kupongezana.
Kwa habari zaidi Bofya na Endelea........

0 comments:

Post a Comment