SONYA_FLAWLESS_IMG
WE CREATE GREATNESS. | Professional Networker | Global Business Builder | Health And Wellness Coach | YOUR DREAM OUR PLAN.

Thursday, October 3, 2013

Mkutano wa 23 wa Mwaka wa Wanachama na Wadau wa Mfuko wa Pensheni wa PPF waendelea leo kwa siku ya pili

Mwenyekiti wa Kikao cha kwanza cha Mkutano wa 23 wa Mwaka wa Wanachama na Wadau wa Mfuko wa Pensheni wa PPF iliyokuwa ikihusu Ukubwa wa mifuko ya hifadhi za jamii,Daud Msangi akitoa muongozo kwa Wadau wa PPF waliopo kwenye mkutano huo,kabla ya kumuita mtoa Mada.
Mtoa Mada wa kwanza iliyokuwa ikihusu Ukubwa wa mifuko ya hifadhi za jamii katika Sekta isiyo rasmi, Dominic Muindi ambaye ni Mtaalamu wa Mifuko ya Hifadhi ya Jamii kutoka nchini Kenya akiwasilisha mada yake hiyo kwa Wanachana na Wadau PPF waliopo kwenye Mkutano wa 23 wa Mwaka wa Wanachama na Wadau wa Mfuko wa Pensheni wa PPF,unaendelea kufanyika kwenye ukumbi wa Kimataifa wa Mikutano wa AICC,jijini Arusha leo.
Mchangia Mada iliyokuwa ikihusu Ukubwa wa mifuko ya hifadhi za jamii katika Sekta isiyo rasmi,Dk. Saqware Abdallah Naniyo akifafanua maswala mbali mbali yahusuyo mada hilo iliyowasilishwa na Mtaalamu wa Mifuko ya Hifadhi ya Jamii kutoka nchini Kenya,Ndg. Dominic Muindi katika Mkutano wa 23 wa Mwaka wa Wanachama na Wadau wa Mfuko wa Pensheni wa PPF unaendelea kufanyika kwenye ukumbi wa Kimataifa wa Mikutano wa AICC,jijini Arusha leo.
Mbunge wa Jimbo la Busega,Mh. Titus Kamani akiuliza swali kwa mtoa Mada hiyo.
Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Pensheni wa PPF,William Erio akizungumza jambo wakati wa Mkutano huo.
Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Maendeleo ya Jamii na Mbunge wa Jimbo la Peramiho,Mh. Jenista Mhagama akichambia mada iliyowasilishwa na Mtaalamu wa Mifuko ya Hifadhi ya Jamii kutoka nchini Kenya,Ndg. Dominic Muindi kutoka nchini Kenya (hayupo pichani) wakati wa Mkutano wa 23 wa Mwaka wa Wanachama na Wadau wa Mfuko wa Pensheni wa PPF,unaendelea kufanyika kwenye ukumbi wa Kimataifa wa Mikutano wa AICC,jijini Arusha leo.
Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali na Mbunge wa Jimbo la Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe, akizungumza kwenye mkutano huo.
Mwenyekiti wa Chama cha Wafanyakazi Cha Taasisi ya Elimu ya Juu,Yusuph Singo akiuliza maswali kadhaa kwa Mtoa Mada,wakati wa Mkutano wa 23 wa Mwaka wa Wanachama na Wadau wa Mfuko wa Pensheni wa PPF,unaendelea kufanyika kwenye ukumbi wa Kimataifa wa Mikutano wa AICC,jijini Arusha leo.
Mkurugenzi wa Rasilimali Watu wa DAWASA,Mary Ntukule akiuliza swali kwenye Mkutano huo.
Mjumbe wa bodi ya Wadhamini ya Mfuko wa Pensheni wa PPF,Frank Mtosho akifafanua jambo juu ya mada iliyokuwa ikitolewa na Mtaalamu wa Mifuko ya Hifadhi ya Jamii kutoka nchini Kenya,Ndg. Dominic Muindi (hayupo pichani),wakati wa Mkutano wa 23 wa Mwaka wa Wanachama na Wadau wa Mfuko wa Pensheni wa PPF,unaendelea kufanyika kwenye ukumbi wa Kimataifa wa Mikutano wa AICC,jijini Arusha leo.
Mwanachama wa Mfuko wa Pensheni wa PPF, ambaye ni mstaafu wa serikalini,Mzee Samson Kibonde akielezea namna anavyoweza kumudu maisha yake katika mazingira ya ustaafu na kusema amefurahia maisha yake kutokana na kufaidi mafao anayopokea kutoka PPF.
Naibu Waziri wa Kazi na Ajira,Mh. Dk. Makongoro Mahanga akifatilia mada mbali mbali zinazoendelea kuwasilishwa kwenye Mkutano wa 23 wa Mwaka wa Wanachama na Wadau wa Mfuko wa Pensheni wa PPF,unaendelea kufanyika kwenye ukumbi wa Kimataifa wa Mikutano wa AICC,jijini Arusha leo.
Mbunge wa Jimbo la Ludewa,Mh. Deo Filikunjombe akifatilia Mkutano huo kwa Umakini.
Mkurugenzi wa Zamani wa Mfuko wa Pensheni wa PPF,David Mataka akifatilia Mkutano huo.
Wajumbe wa bodi ya Wadhamini ya Mfuko wa Pensheni wa PPF,kutoka kushoto, Baraka Igangula, Nassoro Baeaza na Frank Mtosho, wakifuatilia mada iliyokuwa ikitolewa na Mtaalamu wa Mifuko ya Hifadhi ya Jamii kutoka nchini Kenya,Ndg. Dominic Muindi (hayupo pichani),wakati wa Mkutano wa 23 wa Mwaka wa Wanachama na Wadau wa Mfuko wa Pensheni wa PPF,unaendelea kufanyika kwenye ukumbi wa Kimataifa wa Mikutano wa AICC,jijini Arusha leo.
Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Pensheni wa PPF,William Erio,Naibu Waziri wa Kazi na Ajira,Mh. Dk. Makongoro Mahanga pamoja na Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Maendeleo ya Jamii na Mbunge wa Jimbo la Peramiho,Mh. Jenista Mhagama wakifatilia Mkutano huo.

Mbunge wa Jimbo la Busega,Mh. Titus Kamani (kushoto) akiteta jambo na Mbunge wa Jimbo la Mkanyageni,Mh. Habib Mnyaaa.
Mtoa Mada mwingine iliyokuwa ikihusu Umuhimu wa Pensheni hasa Baada ya Kustaafu,Dk. Godwin Kaganda akiwasilisha mada yake hiyo.
Mkurugenzi wa Fedha wa Mfuko wa Pensheni wa PPF,Martin Mmari akitia Taarifa ya Mwaka ya Fedha ya Mfuko huo.
Meneja Uratibu wa Kanda wa Mfuko wa Pensheni wa PPF,Mbaruku Magawa (Kushoto) na Meneja wa Kitengo cha Sheria cha Mfuko huo,Nikenda Kileo, wakifuatilia mada zilizokuwa zikitolewa.

Wakurugenzi wa Idara mbali mbali za Mfuko wa Pensheni wa PPF wakifatilia mada kwenye Mkutano huo.
Sehemu ya Wanachama na Wadau wa Mfuko wa Pensheni wa PPF waliohudhulia Mkutano huo wa Mwaka wa Wadau wa PPF,unaendelea kufanyika kwenye ukumbi wa Kimataifa wa Mikutano wa AICC,jijini Arusha leo.
CHANZO MICHUZI MATUKIO

0 comments:

Post a Comment