SPIKA
wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Anne Makinda
akionyesha kwa waandishi wa habari ripoti ya timu ya Bunge kuhusu
ufuatiliaji wa hukumu ya malipo ya rada kutoka kwa kampuni ya BAE ya
nchini Uingereza. Mkutano huo na waandishi wa habari umefanyika leo
(jana) Bungeni mjini Dodoma
SPIKA
wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Anne Makinda
akipokea ripoti ya timu ya wabunge wa Bunge la Muungano wa Tanzania
kutoka kwa Kiongozi wa timu hiyo ambaye ni Naibu Spika Mhe. Job Ndugai.
Timu hiyo ilikwenda nchini Uingereza kufuatilia hukumu ya malipo ya
fedha za rada kutoka katika ya British Aerospace (BAE ) ya nchi humo
ambayo inadaiwa na Serikali ya Tanzania kiasi cha zaidi ya Tsh.
Bilioni 80. Mkutano huo na waandishi wa habari umefanyika leo (jana)
Bungeni mjini Dodoma.
KIONGOZI
wa timu ya Bunge iliyofuatilia hukumu ya malipo ya rada ambaye ni Naibu
Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Job Ndugai
(katikati) akitoa taarifa ya ujumbe wa timu hiyo katika ukumbi wa
mikutano Bungeni mijini Dodoma. Kulia kwake ni mjumbe wa timu Mhe.
Angela Kairuki (Viti Maalum) na kushoto ni Mussa Azzan Zungu (Ilala).
Picha zote na Islamail Ngayonga-MAELEZO.
0 comments:
Post a Comment