SONYA_FLAWLESS_IMG
WE CREATE GREATNESS. | Professional Networker | Global Business Builder | Health And Wellness Coach | YOUR DREAM OUR PLAN.

Wednesday, July 6, 2011

Timu Ya Wabunge iliyoongozwa na Naibu Spika Job Ndugai Kufwatilia Hukumu ya Malipo ya Rada Kutoka Kampuni ya BAE ya nchini Uingereza Yawasilisha Ripoti Yake Kwa Spika Anne Makinda Leo

SPIKA wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Anne Makinda  akionyesha kwa waandishi wa habari ripoti ya timu ya Bunge kuhusu ufuatiliaji wa hukumu ya malipo ya rada kutoka kwa kampuni ya BAE ya nchini Uingereza. Mkutano huo na waandishi wa habari umefanyika leo (jana) Bungeni mjini Dodoma
SPIKA wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Anne Makinda akipokea ripoti ya timu ya wabunge wa Bunge la Muungano wa Tanzania kutoka kwa Kiongozi wa timu hiyo ambaye ni Naibu Spika Mhe. Job Ndugai. Timu hiyo  ilikwenda nchini Uingereza kufuatilia hukumu ya malipo ya fedha za rada kutoka katika ya British Aerospace (BAE ) ya nchi humo ambayo inadaiwa na Serikali ya Tanzania kiasi cha zaidi ya Tsh. Bilioni 80. Mkutano huo na waandishi wa habari umefanyika leo (jana) Bungeni mjini Dodoma.
KIONGOZI wa timu ya Bunge iliyofuatilia hukumu ya malipo ya rada ambaye ni Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano  wa Tanzania, Job Ndugai (katikati) akitoa taarifa ya ujumbe wa timu hiyo katika ukumbi wa mikutano Bungeni mijini Dodoma. Kulia kwake ni mjumbe wa timu Mhe. Angela Kairuki (Viti Maalum) na kushoto ni Mussa Azzan Zungu (Ilala).
Picha zote na Islamail Ngayonga-MAELEZO.

0 comments:

Post a Comment