SONYA_FLAWLESS_IMG
WE CREATE GREATNESS. | Professional Networker | Global Business Builder | Health And Wellness Coach | YOUR DREAM OUR PLAN.

Thursday, July 14, 2011

Kenya Kufungua Kambi Ya Ifo II


Waziri Mkuu Raila Odinga
Serikali ya Kenya imeamuru kufunguliwa kwa kambi ya Ifo kaskazini mashariki mwa Kenya ambako maelfu ya watu wanawasili kila siku wakikimbia ukame na mzozo nchini Somali.
Amri hii imetolewa na Waziri Mkuu wa Kenya Raila Odinga aliyetembelea kambi ya wakimbizi ya Dadaab ambayo ni kambi kubwa zaidi ya wakimbizi duniani , ikiwahifadhi wakimbizi zaidi ya elfu mia tatu na mia nane, idadi ambayo ni kubwa kuliko uwezo wa kambi hiyo.
Serikali ya Kenya ilikuwa imekabiliwa na shinikizo kutoka kwa jumuiya ya kimataifa kufungua kambi nyingine lakini ikawa na hofu juu ya usalama wa nchi na kuhofia kwa wakimbizi hao wakejenga makao ya kudumu nchini Kenya.

0 comments:

Post a Comment