Waziri Mkuu Raila
Odinga
Serikali ya Kenya imeamuru kufunguliwa kwa kambi ya Ifo
kaskazini mashariki mwa Kenya
ambako maelfu ya watu wanawasili kila siku wakikimbia ukame na mzozo nchini
Somali.
Amri hii imetolewa na
Waziri Mkuu wa Kenya
Raila Odinga aliyetembelea kambi ya wakimbizi ya Dadaab ambayo ni kambi kubwa
zaidi ya wakimbizi duniani , ikiwahifadhi wakimbizi zaidi ya elfu mia tatu na
mia nane, idadi ambayo ni kubwa kuliko uwezo wa kambi hiyo.
Serikali ya Kenya ilikuwa imekabiliwa na shinikizo kutoka
kwa jumuiya ya kimataifa kufungua kambi nyingine lakini ikawa na hofu juu ya
usalama wa nchi na kuhofia kwa wakimbizi hao wakejenga makao ya kudumu nchini Kenya .
0 comments:
Post a Comment