Shaggy.
Na Andrew Chale, Zanzibar.
KUTUA NA BOTI MAALUM VISIWANI ZANZIBAR.
Mwanamuziki
wa kimataifa wa ragga na mshindi wa tuzo za Grammy 2011, Orville
Richard ‘Shaggy’ usiku wa leo anatarajia kupanda jukwaani ndani ya
Ngome kongwe ukumbi wa Mambo kutumbuiza shoo kali huku akisindizwa na
wanamuziki nyota wa hapa nchini sambamba na kundi la THT Dancers.
Kwa
mujibu wa Meneja masoko na mmoja wa waratibu wa Tamasha la Filamu za
Nchi za majahazi maarufu ZIFF, Laurian Kipeja alisema kuwa,
mwanamuziki huyo wa kimataifa atapanda jukwaani hiyo majira ya usiku
na kupiga shoo kali na ya aina yake huku akisindikizwa na wasanii
mahiri wa hapa nchini.
Kipeja
alisema kuwa, tayari tiketi za shoo hiyo zimeanza kutolewa katika
ofisi zilizopo makao makuu ya ZIFF ndani ya Ngome Kongwe huku bei zikiwa
nafuu kwa kila mmoja.
“Shoo
hii itakuwa ni ya pekee na ya aina yake kwa wakazi wa Zanzibar na
wageni mbalimbali huku kima cha juu kwa V.I.P. wa juu ni laki moja
(100000) na V.I.P wa kawaida (50,000) na vya kawaida kwa wageni ni
30,000 huku wazawa ama wakazi ni 15,000” alisema Laurian.
Aidha,
inadaiwa Shaggy atatua visiwani hapa na boti maalum mapema leo na
kisha saa sita mchana atafanya mkutano na vyombo vya habari sambamba na
kufunga vyombo kwenye hoteli ya Zanzibar Resort.
Kwa
upande wake,meneja wa ZIFF, Danny Nyalusi alisema wasanii watakao
msindikiza Shaggy ni pamoja na Sultan King, na kundi la THT ambapo
watapiga shoo kali ambayo haijawai kutokea visiwani humo.
Pia
alisema kuwa kwa mwaka huu, kaulimbiu ya ZIFF imebeba ujumbe wa ‘A
SEASON OF VISIONS’ na kwa mara ya kwanza, tamasha hilo limedhaminiwa
na mdhamini mkuu Kampuni ya Bia ya Serengeti, kupitia kinywaji chake
cha Tusker Malt, Prime Time promotion, Coconut FM, Azam Marine Co ltd,
TTB, Common Wealth Foundation, Coca-Cola, GIZ (TZ), na Ujerumani, Smole,
Movenpick, Kituo cha Utamaduni cha Ufaransa.
0 comments:
Post a Comment