Makamu
wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal
akimkabidhi Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais mahusiano na Uratibu Stephen
Wassira Tuzo ya UN ya mshindi wa pili ya Tanzania katika kutoa huduma
bora kwa Jamii (Mkurabita) wakati Makamu alipofika kwenye Ukumbi wa
Mlimani City jijini Dar es Salaam Juni 23, 2011 kufunga maadhimisho ya
siku ya Utumishi ya Umoja wa Mataifa na Afrika, ikiwa ni mara ya kwanza
kwa hafla hiyo kuadhimishwa Barani Afrika na kufanyika nchini Tanzania.
Walipata tuzo hawa ni kutoka Ubalozi wa Afrika ya Kusini, wakifurahia tuzo yao kwa pamoja baada ya kukabidhiwa.
Balozi wa canada nchini, akipokea tuzo kwa niaba ya nchi yake.
Zoezi la kukabidhi tuzo linaendelea kwa wawakilishi wa nchi mbalimbali.
Wafanyakazi wa Ubalozi wa Afrika ya Kusini nchini, wakifurahia tuzo yao baada ya kukabidhiwa.
Baadhi
ya watu kutoka mataifa mbalimbali walioshiriki wakati wa hafla hiyo ya
kutoa tuzo na kufunga maadhimisho hayo katika Ukumbi wa Mlimani City Dar
es Salaam.
(Picha na Muhidin Sufiani-OMR).
0 comments:
Post a Comment