Afisa
Mkuu wa Masoko na Mahusiano wa Vodacom Tanzania Mwamvita Makamba
katikati akiongea na waandishi wa habari wakati wa kusaini mkataba wa
shilingi Milioni 40, zilizotolewa na Vodacom Foundation kwa CCBRT kwa
ajili ya ujenzi wa wodi ya wanawake na watoto katika hospitali mpya ya
CCBRT Boabab. Kushoto Afisa Mtendaji Mkuu wa CCBRT Erwin
Telemans,watatu toka kushoto Meneja Mahusiano wa CCBRT Kira Thomas na
Mkuu wa Vodacom Foundation Yessaya Mwakifulefule.
Afisa
Mtendaji Mkuu wa Hospitali ya CCBRT Erwin Telemans kushoto, Afisa Mkuu
wa Masoko na Mahusiano wa Vodacom Tanzania Mwamvita Makamba wakisaini
makubaliano ya Vodacom Foundation kuchangia shilingi Milioni 40 za
ujenzi wa wodi ya wanawake na watoto kwenye Hospitali mpya ya CCBRT
Boabab itakayojengwa jijini Dar es salaam. Wanaoshuhudia katikati Mkuu
wa Vodacom Foundation Yessaya Mwakifulefule na kulia Meneja Mahusiano wa
CCBRT Kira Thomas.
Afisa
Mtendaji Mkuu wa Hospitali ya CCBRT Erwin Telemans kushoto
akipokea mkataba kutoka kwa Afisa Mkuu wa Masoko wa Kampuni ya Vodacom
Tanzania Mwamvita Makambawa Vodacom kwa ajili ya kuchangia shilingi
milioni arobaini katika ujenzi wa wodi ya wanawake na watoto kwenye
hospitali maalum ya wanawake itakayojengwa jijini Dar es salaam.Kulia
ni Meneja Mahusiano wa CCBRT Kira Thomas .
Afisa
Mkuu wa Masoko na Mahusiano wa Vodacom Tanzania Mwamvita Makamba
(kulia) Mkuu wa Vodacom Foundation Yessaya Mwakifulefule wakimwangalia
Afisa Mtendaji Mkuu wa Hospitali ya CCBRT Erwin Telemans (kushoto)
akisoma mkataba wa makabadhiano ya shilingi Milioni Arobaini kutoka
Vodacom zitakazotumika katika ujenzi wa jengo la wanawake na watoto
katika Hospitali ya CCBRT Baobab.
0 comments:
Post a Comment