SONYA_FLAWLESS_IMG
WE CREATE GREATNESS. | Professional Networker | Global Business Builder | Health And Wellness Coach | YOUR DREAM OUR PLAN.

Tuesday, June 7, 2011

TAASISI ZA KIFEDHA ZATAKIWA KUTUMIA FURSA ZILIZOPO VIJIJINI KUWEKEZA!!

Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Jordan Rugimbana kwa niaba ya Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam  akifungua warsha kuhusu Mahitaji na Vikwazo katika Upatikanaji wa Huduma za Kifedha Tanzania iliyofanyika leo jijini Dar es Salaam katika kituo cha Utafiti cha ESRF, ambapo amewataka wasomi na wataalam nchini kutumia matokeo ya tafiti mbalimbali kuisadia Serikali katika kutimiza malengo ya kimaendeleo haswa katika kuboresha sekta ya huduma za kifedha. Kulia ni Mkurugenzi Mtendaji wa Kituo cha ESRF Bohela Lunogelo na kushoto ni Katibu Tawala wa Mkoa Theresia Mmbando.
Mkurugenzi Mtendaji wa Kituo cha ESRF Bohela Lunogelo akimkaribisha mgeni rasmi kufungua warsha hiyo ambapo amefafanua lengo kuu la utafiti huo kuwa ni kutoa msaada wa serikali, watunga sera, watoa huduma za kifedha kwenye mabenki, taasisi binafsi, watafiti, wasomi na jumuiya ya wafadhili kwa ujumla. Katikati ni mgeni rasmi Jordan Rugimbana na Kushoto ni Katibu Tawala Mkoa Theresia Mmbando.
Wadau kutoka Taasisi mbalimbali wakifuatilia presentation iliyokuwa ikionyesha matokeo ya utafiti huo.
Mmoja wa watafiti Vivian Kazi (kushoto) akiwasilisha presentation ya kwanza ya utafiti wa FinScope 2009 juu ya mahitaji na vikwazo katika upatikanaji wa huduma za kifedha nchini. Huu ni utafiti wa pili wa aina hii kufanyika Tanzania ambapo wa kwanza ulifanyika mwaka 2006. Katikati ni Mkurugenzi Mtendaji Msaidizi wa ESRF  Dkt. Donatila Kaino.
Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Utafiti juu ya Masuala ya Kiuchumi  na Kijamii Tanzania (ESRF) Bohela Lunogelo (wa kwanza kulia waliokaa) katika picha ya pamoja na washiriki wa warsha ya Mahitaji na Vikwazo katika Upatikanaji wa Huduma za Kifedha nchini Tanzania.

0 comments:

Post a Comment