Rais wa shirikisho la soka duniani Fifa Sepp Blatter anatarajiwa
kushinda muhula wake wanne baada ya wale waliotaka kuahirishwa kwa uchaguzi huo
kushindwa kusimamisha.
wanamfalme wa Uingereza William ameunga mkono msimamo wa
shirikisho la soka la England na lile la Scotland kuwa uchaguzi wa huru na haki
hauwezi kufanyika huku kukiwa na madaia ya ufisadi.
Blatter ndiye mgombea pekee kwa kuwa mpinzani wake Mohammed bin
Hammam amesimamishwa.
Wakati huo huo, Chuck Blazer,katibu mkuu wa shirikisho la soka
la Concacaf, amenusurika kutimuliwa kama katibu mkuu.
Madai ya ufisadi ya Blazer yamesababisha wajumbe wawili
wakuu,akiwemo Mohammed bin Hamman, kusimamishwa kuhudumu katika shirikisho
hilo.
Mashirikisho ya FA na SFA yamejaribu kutafutwa kuungwa mkono
katika pendekezo lao la kutaka uchaguzi kusitishwa.
Mashirikisho mengine kutoka Uingereza,ikiwemo shirikisho la
Wales na lile la Ireland,yanaonekana hayako tayari kuunga mkono majirani zao.
Ili kuweza kusitisha uchaguzi wa Jumatano,inahitaji mataifa 150
kati ya 208 kupiga kura kuunga mkono hatua hio,jambo ambalo mwenyekiti wa
shirikisho la FA David Bernstein haoni likiwezekana.
Na kwa kuwa tayari wameamua kutoshiriki katika
upigaji kura, Bernstein amesema ni muhimu kwa FA kuweka msimamo wake wazi.
0 comments:
Post a Comment