SONYA_FLAWLESS_IMG
WE CREATE GREATNESS. | Professional Networker | Global Business Builder | Health And Wellness Coach | YOUR DREAM OUR PLAN.

Sunday, May 1, 2011

SHEREHE ZA SIKU YA WAFANYAKAZI DUNIANI-DAR

Baadhi ya wafanyakazi wa Ofisi ya Makamu wa Rais wakipita na bango lenye ujumbe mbele ya mgeni rasmi Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Mecky Sadiki, jukwaa kuu wakati wa sherehe za maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi Duniani Mei Mosi zilizofanyika kwenye Viwanja vya Mnazi Mmoja Dar es Salaam leo. Sherehe hizo Kitaifa zilifanyika Mkoano Morogoro ambapo mgeni rasmi alikuwa ni Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Jakaya Kikwete.
Mmoja wa wafanyakazi ambaye hakuweza kufahamika jina lake akiwa bize kushona kitambaa cha uzi wakati akiwa kwenye viwanja vya Mnazi Mmoja Dar es Salaam jana katika sherehe za maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi Duniani (Mei Mosi).
Sherehe hizo zilifanyika kitaifa mkoani Morogoro.
Wafanyakazi wakiandamana kuelekea katika Viwanja vya Mnazi Mmoja Dar es Salaam leo wakati wa sherehe za maadhimisho ya siku ya Wafanyakazi Duniani (Mei Mosi).
Sherehe hizo ziliadhimishwa kitaifa Mkoani Morogoro na kuhudhuliwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Jakaya Kikwete.
Wafanyakazi wa Tawi la Kampuni ya Tuico, wakipita mbele ya Jukwaa kuu na mabango yao yenye Ujumbe wakati wa sherehe za maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi Duniani
(Mei Mosi) iliyofanyika kwenye Viwanja vya Mnazi Mmoja Dar es Salaam leo na kuhudhuriwa na Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Mecky Sadiki. Sherehe hizo zilifanyika kitaifa mkoani Morogoro ambapo mgeni rasmi alikuwa ni Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Jakaya kikwete.
(Picha na Muhidin Sufiani-VPO).
Na Mo Blog

0 comments:

Post a Comment