SONYA_FLAWLESS_IMG
WE CREATE GREATNESS. | Professional Networker | Global Business Builder | Health And Wellness Coach | YOUR DREAM OUR PLAN.

Sunday, May 1, 2011

RAIS JAKAYA AWAAPISHA MANAIBU KATIBU WAKUU IKULU DAR JANA

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Jakaya Kikwete, akimwapisha John Thomas Mngodo kuwa Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi wakati wa hafla fupi ya kuapishwa Manaibu Katibu Wakuu iliyofanyika kwenye Viwanja vya Ikulu jijini Dar es Salaam jana.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Jakaya Kikwete, akimwapisha Anna Maembe kuwa Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto, wakati wa hafla fupi ya kuapishwa Manaibu Katibu Wakuu iliyofanyika kwenye Viwanja vya Ikulu jijini Dar es Salaam jana.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Jakaya Kikwete, akimwapisha Sihaba Nkinga kuwa Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, wakati wa hafla fupi ya kuapishwa Manaibu Katibu Wakuu iliyofanyika kwenye Viwanja vya Ikulu jijini Dar es Salaam jana.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Jakaya Kikwete akimwapisha Charles Amos kuwa Naibu Katibu Mkuu wa Ofisi ya Waziri Mkuu wakati wa hafla fupi ya kuapishwa Manaibu Katibu Wakuu iliyofanyika kwenye Viwanja vya Ikulu jijini Dar es Salaam jana.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Jakaya Kikwete akimwapisha Alphayo Kidata Ikulu (nafasi moja) wakati wa hafla fupi ya kuapishwa Manaibu Katibu Wakuu iliyofanyika kwenye Viwanja vya Ikulu jijini Dar es Salaam jana.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Jakaya Kikwete akimwapisha Hab Mkwizu kuwa Naibu Katibu Mkuu wa Ofisi ya Rais Menejiment ya Utumishi wa Umma wakati wa hafla fupi ya kuapishwa Manaibu Katibu Wakuu iliyofanyika kwenye Viwanja vya Ikulu jijini Dar es Salaam jana.
Rais Jakaya Kikwete Makamu wake Dkt Mohamed Gharib Bilal wakipiga picha ya kumbukumbi na Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Ulinzi na JKT, Eng. Mussa Ibrahim akiwa na familia yake baada ya kuapishwa rasmi jana.
Rais Jakaya Kikwete akifurahia jambo na Waziri wa Ujenzi Mh. John Pombe Maghufuli, wakati wa hafla ya kuwaapisha Manaibu Katibu Wakuu Ikulu Dar es Salaam jana..
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Jakaya Kikwete akifurahia na mtoto Irene Simba ambaye ni mtoto wa Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi Mwamini Juma Malemi (kushoto) wakati wa hafla fupi ya kuwaapisha Manaibu Katibu Wakuu iliyofanyika kwenye Viwanja vya Ikulu Dar es Salaam jana.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt Jakaya Kikwete, akiwa katika picha ya pamoja na Familia ya Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi Mwamini Juma Malemi baada ya kuapishwa rasmi kwenye hafla iliyofanyika kwenye Viwanja vya Ikulu Dar es Salaam jana.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt Jakaya Kikwete akiwa katika picha ya pamoja na Familia ya Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto Anna Maembe baada ya kuapishwa rasmi leo kwenye hafla iliyofanyika kwenye Viwanja vya Ikulu Dar es Salaam.
(Picha na Muhidin Sufiani- Ofisi ya Makamu wa Rais).

0 comments:

Post a Comment