SONYA_FLAWLESS_IMG
WE CREATE GREATNESS. | Professional Networker | Global Business Builder | Health And Wellness Coach | YOUR DREAM OUR PLAN.

Saturday, May 21, 2011

Rais Mpya Wa Ivory Coast Ameapishwa!!

 Alassane Ouattara 
Miezi sita baada ya uchaguzi uliokuwa na mzozo, rais mpya wa Ivory Coast, Alassane Ouattara, ameapishwa.
Sherehe zilizofanywa mji mkuu, Yamoussoukro, zilihudhuriwa na viongozi wengi wa Afrika pamoja na Rais Sarkozy wa Ufaransa na Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Ban Ki-Moon.
Bwana Uottara aliushukuru ulimwengu kwa kumuunga mkono , na alisema kwamba kauli ya wananchi wa Ivory Coast imeshinda.
Piya alitoa wito kwa watu kuonesha udugu na mapatano, na aliahidi kuwa ataongoza kwa niaba ya taifa zima.
Mwandishi wa BBC mjini Abidjan anasema, kazi kubwa inayomkabili Bwana Outtara ni usalama na uchumi.

0 comments:

Post a Comment