SONYA_FLAWLESS_IMG
WE CREATE GREATNESS. | Professional Networker | Global Business Builder | Health And Wellness Coach | YOUR DREAM OUR PLAN.

Saturday, April 16, 2011

Wema Atiwa Mbaroni

NaGladness Mallya na Haruni Sanchawa
Kwa mara nyingine Miss Tanzania ‘The history’ 2006/07 ambaye kwa sasa ni moto wa kuotea mbali katika Bongo Movies, Wema Abraham Sepetu, ameshikiliwa na polisi katika Kituo cha Oysterbay Kinondoni, Dar es Salaam kwa saa kadhaa kwa ajili ya mahojiano.
Uchunguzi wa Risasi Jumamosi umefanikisha kupatikana kwa chanzo cha mrembo huyo kushikiliwa na ‘wajeda’ kuwa ni kutoa lugha chafu na vitisho kwa Prodyuza wa Studio na Lebo ya Sharobaro, Rahim Rummy Nanji ‘Bob Junior’.
Akizungumza na gazeti hili jijini Dar juzi, Bob Junior alidai kuwa Aprili 11, mwaka huu saa 12 jioni, Wema alimpigia simu na kumporomoshea mvua ya matusi makubwa ikijaziwa na vitisho vya kufa mtu.
Rais huyo wa Masharobaro aliendelea kushusha tuhuma kuwa, mbali na kumtishia aliahidi kumtafutia mabaunsa ili ‘wamruke ukuta’ jambo ambalo hakuwa tayari kukutana nalo hivyo aliona njia pekee ya kukwepa ‘sheshe’ hilo ni kukimbilia polisi.
Bob Junior alisema alimfungulia Wema jalada la kesi namba OB/RB/6337/2011-KUTISHIA MAISHA.
WEMA CHINI YA ULINZI
Ilielezwa kwamba, baada ya Bob Junior kufungua kesi hiyo, Wema naye alifika kituoni hapo kwa nia ya kufungua kesi kwa ajili ya rais huyo wa masharobaro ambapo aliambiwa na polisi kuwa yuko chini ya ulinzi kwa mahojiano.
Wema alidaiwa kukaa kituoni kwa zaidi ya saa 3, Aprili 13, mwaka huu hadi alipofika mwimbaji wa FM Academia ‘Wazee wa Ngwasuma’, Patcho Mwamba na kumwekea dhamana.
Wema aliachiwa huru kwa masharti ya kuripoti kituoni hapo Aprili 14, mwaka huu saa 2:30 asubuhi.
Risasi Jumamosi lilifika kituoni hapo na kumshuhudia Wema akitinga eneo hilo saa 3:30 asubuhi akifuatana na wasanii wenzake wa filamu, Rose Donatus Ndauka na Jacqueline Steven Pentezel ‘Jack wa Chuz’.
Hata hivyo, mapaparazi wetu walipojaribu kuzungumza nao, Jack wa Chuz alijibu kwa niaba ya Wema aliyegoma kuzungumza na kusema kuwa walifika eneo hilo kuchukua kibali cha ‘kushuti’ filamu.
Habari za ndani zilidai kuwa, Wema na Bob Junior walikalishwa chini kituoni hapo na kutakiwa kumaliza tofauti zao lakini prodyuza huyo alikataa na kutaka ishu iende mahakamani.
KWA NINI WEMA NA BOB JUNIOR?
Chanzo cha yote hayo ni bifu linaloendelea kati ya Bob Junior na msanii Naseeb Abdul ‘Diamond’ ambaye ni laaziz wa Wema ikielezwa kuwa prodyuza huyo alimdhalilisha mrembo huyo hivyo naye akataka kulipiza.
Mara ya kwanza Wema alikaa nyuma ya nondo za mahabusu mwaka 2009 akikabiliwa na shitaka la kuvunja kioo cha gari la staa wa filamu, Steven Charles Kanumba.
BOFYA HAPA

0 comments:

Post a Comment